gorretti54
Member
- Jun 21, 2012
- 53
- 17
Sijakuelewa hapo kujiunga na nyinyi ni bure. BURE kivipi? Hata forever living ni bure lakini ni lazima ununue products ili uwe member. Unaweza kujiunga bure halafu iweje?unakaa bila kununua products? GNLD najua ndiyo huwa kuna joining fee na fee ya ku renew kila mwaka. Ndugu yangu katika kusaka mafanikio hakuna kitu kirahisi ama sivyo kila mtu angekuwa tajiri hapa duniani. Lakini matajiri ni kiduchu tu na itaendelea kuwa hivyo mpaka mwisho wa nyakati.Mimi sipondi kampuni zingine wala yenu hapa natoa facts ndugu....bado hujaboreka na kukata tamaa vizuri kuna vitu vingi sana navijua ambavyo nyie hamvijui na hao ma upliner wenu wanawaficha sana wanakula hela zenu nyingi tu.....ukivijua utakuja kumwaga kilio kipindi hicho ushapoteza pesa nyingi na muda (yetu macho, tuombe uhai).... ni vile design nashindwa kuviandika hapa....ni vya kuelezewa kwa ukaribu zaidi. Kama huamini hujawahi kujiuliza kwanini some forever living top distributors wa nigeria hawapendi kusema ni mbinu gani wanatumia biashara zao za flp zinafanikiwa ?? Kuna watu hapa Tanzania wanajua sema wameuchuna tu...kwanza kujiunga na sisi ni BURE. Sisi tumejipanga na tutahakikisha Network Marketing ina pata jina zuri na kubwa Tanzania na Africa yote kwa ujumla...enough is enough, Hatutaki kuona watu wananyanyasika tena !! kuhusu bidhaa kutengenezwa na top doctors na leading experts sioni tatizo kubwa...kama kweli kitu kimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu na kimezibitishwa na mashirika makubwa ya kisayansi...kwanini usitangaze kwa watu sasa ?? na certificates tunazo za kutosha tu... Lazima mtu ajue anatumia kitu cha quality kubwa na kwa bei nafuu sio bla bla nyingi. Personal development na goal setting ni vitu vizuri lakini mazingira ya kazi nayo yaruhusu basi....ni sawa sawa unafanya mazoezi ya pumzi then unapewa kazi ya kubeba mizigo mizito (completely inverse/ no correlation). Maisha yako hayatabadilika kama usipo jaribu jifunza ukweli ninaokwambia (si shangai mimi nilikua kama wewe hapo awali)...for more details about my business ni PM.
Goodluck.
Mimi nadhani labda ulikuwa na upline mbaya wakati upo FLP au wewe ni mtu wa kukata tamaa mapema kabla hujajifunza kila kitu na labda vilevile unataka kupata mafanikio kirahisirahisi.
Mbona ma upline wengi wanatoa masaada mkubwa sana kwa downlines...kwenye biashara ya network marketing bila ya kumsaidia na kumpa ujanja downline wako wewe utafanikiwa vipi?
Top distributor wa flp africa(John Ekperigin) nilikwenda kumuona mwenyewe JB belmont hotel alipokuja na jamaa alieleza vitu vizuri tu. Nataka unijibu hili swali. Hivi kwenye network marketing unaweza kufanikiwa vipi bila kuwa coach downlines wako wa copy kile unachokifanya wewe?
Hii siyo biashara ya chapati ya kufichana siri ya viungo. Hii ni biashara ya kushikana mkono, kuleana, kusaidiana mpaka hapo downline wako atakapoweza kusimama mwenyewe na yeye kuanza kuduplicate tricks and techniques zako kwa downlines wake. Duplication of Efforts.
Mimi nadhani unahitaji kutulia hata kwenye hiyo kampuni yako. Nadhani kinacho count sanavkwenye hii biashara sidhani ni ubora wa bidhaa au marketing plan. Kinachocount sana ni wewe mwenyewe ni mtu wa aina gani. kama ni mtu wa kukimbiakimbia utashindwa tu hata kwenye hiyo kampuni yako mpya. Maana watu wanaofanikiwa kwenye haya makampuni ni wale wanaonaamua kweli kujifunza na kufanya hii biashara kwa jinsi inavyotakiwa.