BOT yadai "Hatujalipa Mabilioni Kisiasa!

Rev.Kishoka

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
4,526
Reaction score
1,552
Kama kuna Jamhuri inayojua kufuja fedha na rasilimali bila kutumia akili ama kwa makusudi, ni jamhuri ya Tanzania.

Serikali iliona ulazima kutumia fedha nyingi kiasi hiki eti kutoa fidia bila uhakiki au uthibitisho. Kila kitu kilifanywa kwa hisia na kufuata mkumbo.

Maswali nililouliza wakati hii Stimuli ilipoanzishwa nayauliza tena na nyongeza! Zaidi ni kuonyesha wazi kuwa kama tuliweza chapisha fedha eti kunusuru ajira za watu 42000 wa sekta binafsi, lakini leo hii tunakataa kuongea kima cha chini tukidai hatuna fedha ni upunguani wa hali ya juu.

Maswali yangu kwa Ndulu na Rais wake Kikwete ni haya:
  1. Fidia hizi zilitolewa kama misaada, mikopo au sadaka? Je ni masharti gani yaliambatanishwa na fidia hizi?
  2. Kama fidia ilikuwa ni msaada wa kugawia mtu fedha kama sadaka, je ni uthibitisho gani kuwa makampuni haya yalipata hasara kwa ajili ya mtikisiko wa mwaka mmoja? Je miaka mingine waliyopata faida ya ziada hawakuwa na limbikizo la mtaji na faida la kutosha ili kumudu kupungua kwa mapato?
  3. Je makampuni haya, yamekuwa yakiliingizia Taifa mapato ya kiasi gani na kodi wanayoilipa ni kiasi gani?
  4. Je fedha hizi za misaada zitaonekana vipi katika mizania (balance sheet) ya makampuni haya na je zitakatwa kodi?
  5. Kwa nini Serikali ilipotenga fungu hili, halikuliweka kama mikopo na kuweka ulazima wa kulipwa na kuhakikiwa kwa fidia hii itakayoonyesha makampuni haya yakitumia hizo fedha kuongeza uzalishaji?
  6. Kwa nini Serikali haikutumia fedha hizi kuboresha miundo mbinu au kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza bidhaa kamili (process industry) ili kupunguza tabia ya Tanzania kupoteza thamani ya mazao yake kwa kwenda kwa madalali? Mfano kama Pamba inalimwa Mwanza, na mkulima anaiuza kwa Ushirika nao unapelekwa kwenye jineri kwa uchambuzi kisha kupeleka nyuzi ulaya, kwa nin Serikali haikutumia nafasi hii kuimarisha uchambuzi wa Pamba kutoka utengenezaji wa nyuzi na pamba iliyochambuliwa na kuwa vitambaa na nguo kamili ili kuongezea Taifa pato na hata kuongeza ajira?
Naomba wasaidizi wa Ndulu na Kikwete mtoke mekoni na mje kujibu maswali yangu!

Kama mtadai eti hata Marekani walitoa Stimuli, nitawapasha hivi, Stimuli ya Marekani haikugawiwa kama peremende, ilikuwa ni mikopo kwa Mabenki ambayo yaliwekewa masharti magumu na muda maalumu wa kurudisha mtaji(mkopo), na serikali ikapunguza kodi za mapato kwa wananchi wake wenye mishahara na kipato fulani na mwisho Serikali ikatumia fedha hizo hizo kwa kuamsha shughuli za uzalishaji mali kwa kutenga fungu maalumu lililolipia gharama za uzalishaji mali huo ambao ni nje ya bajeti ya kawaida ya matumizi!

 
wacha tu yesu arudi kwa mwendoooo huuuuuuuuuuuuuuu
 
PDidy,

TUlikuwa na fedha za kutosha kuiboresha mfumo a Reli ili usafirishaji uendelee bila matatizo. Tulikuwa na fedha za kutosha kuboresha mfumo wa umeme na maji ili uzalishaji uendelee na Serikali iwe na uhakika wa mapato.

Lakini pesa tumewapa Maandazi Tour Company na Changudoa Motel kisa eti watalii kutoka Ugagagigikoko walishindwa kupanda ungo!

Viwanda kila siku vinashidwa kufanya kazi kutokana na ukosefu wa umeme na maji na wanashindwa kusafirisha bidhaa kisa TRL mataruma yamepata pancha lakini hatuoni umuhimu wa kuwekeza kwenye miundo mbinu itakayo hakikisha kuna uzalishaji mali!
 
Tshs. 1.7 TRILLION kunusuru uchumi zinatoka serikalini, Tshs 1.5 BILLION kunusuru reli zinaombwa kwa Gaddafi.....walahiiiiiii tumelogwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…