Bodi ya Uhasibu ahirisheni Mitihani

musami

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2011
Posts
1,434
Reaction score
460
Kutokana na hatua iliyochukuliwa na Bodi ya Uhasibu (NBAA) ya kuamuru vituo vyote vinavyowaandaa Watahiniwa(Tution Providers) kusitisha madarasa hayo, badala yake masomo hayo yaendeshwe kwa njia ya Mtandao(Online Studies)

Katika jitihada ya kukabiliana na Ugonjwa wa Covid-19,wakati huo huo ratiba ya Mtihani wa Mei 2020 iko palepale,pamoja na matatizo haya makubwa ya kusitisha Review classes.Sasa naomba niwaulize watu wa NBAA, hawaoni kwamba ushauri wao wa kuwaambia Tution Providers watumie njia ya Mtandao(Online studies)ni mgumu mno kuutekeleza ?

Ukizingatia kuwa mfumo huo wa ufundishaji, unahitaji maandalizi,ni ghali kwa walimu na watahiniwa (issue ya bando na gharama ya kununua vifaa vya kutumia kama Computer na Simu)kwa kuzingatia kuwa ni jambo lililokuja ghafla.

Nawasihi sana watu wa Bodi mapambano ya Corona ambayo hatujui yataisha lini yasiwe sababu ya kuwaumiza watahiniwa na Tution Providers.Tafadhali sogezeni Mtihani mbele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uhasibu kwa kiingereza ni nini?
 
Mitihani ya bodi yoyote duniani mtahiniwa anapaswa kununua vitabu na kujiandaa na sio kusoma tution

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…