Bodi ya mikopo kwa hili mmechemka

Bodi ya mikopo kwa hili mmechemka

Joined
Apr 18, 2012
Posts
95
Reaction score
213
14906960_1001119833333643_6120554555057602529_n.jpg

UKISIKIA KWAMBA MWENDOKASI BILA UMAKINI UNAUWA ..BASI
KUUWA KWENYEWE NDIO HUKU...

BODI YA MIKOPO/HESLB...

Kwa mujibu wa Bw. Badru, kundi la kwanza linajumuisha wanafunzi waombaji wa mikopo wenye uhitaji maalum kama wenye ulemavu uliothibitishwa na Waganga Wakuu wa Wilaya na yatima ambao katika maombi yao waliwasilisha nakala za vyeti vya vifo zilizothibitishwa na makamishna wa viapo.

“Kundi la pili linajumuisha waombaji wa mikopo ambao baada ya uchambuzi wa taarifa zao walizowasilisha na baada ya kulinganisha na gharama za jumla za masomo yao ya sekondari, wamebainika kuwa wana uwezo mdogo wa kugharamia masomo yao ya elimu ya juu na hivyo kuwa na uhitaji zaidi wa mikopo,” amesema Bw. Badru.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Bw. Badru ametaja kundi la tatu na la mwisho kuwa linajumuisha waombaji wa mikopo ambao wenye ufaulu wa juu katika matokeo yao ya kidato cha sita na wamechaguliwa kujiunga na fani za kipaumbele kwa taifa.

Fani hizo ni Sayansi za Tiba, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, uhandisi wa Kilimo, Mafuta na Gesi na Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
Makundi ya wanafunzi waliopata mikopo

“Hivyo basi, hadi sasa tumetoa mikopo kwa wanafunzi 20,183 wakiwemo wanafunzi yatima 4,321, wenye ulemavu 118, wanafunzi wenye uhitaji waliosomeshwa na taasisi mbalimbali katika masomo ya sekondari (87), wanafunzi wanaosoma kozi za kipaumbele 6,159 na wanafunzi wanaosoma kozi zisizo za kipaumbele lakini wanaotoka kwenye familia duni 9,498,” amefafanua Bw. Badru.

Sababu za kukosa mikopo

Katika mkutano huo, kiongozi huyo wa HESLB pia ameeleza kwa kina sababu nyingine za waombaji 27,053 ambao hawajapangiwa mikopo.
Ametaja sababu hizo kuwa ni pamoja na baadhi ya waombaji (90) kuwa na umri wa zaidi ya miaka 30, waombaji mikopo waliopata udahili kwa sifa linganishi (equivalent qualifications) na waombaji waliomaliza masomo ya kidato cha sita zaidi ya miaka mitatu iliyopita.

Kundi jingine la waombaji waliokosa mikopo katika awamu ya kwanza ni waombaji waliopata nafasi katika vyuo kwa ufaulu wa mitihani waliyofanya kama watahiniwa binafsi (Private Candidates) na waombaji ambao hawakurekebisha fomu zao za maombi ingawa waliitwa kufanya hivyo.

Nafasi ya rufaa na uhakiki wa wanafunzi wanaoendelea na masomo
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji huyo pia amewataka waombaji ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo unaotangazwa, kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao utakaofunguliwa kuanzia katikati ya wiki ijayo.

“Tunafahamu kuwa kuna baadhi ya wanafunzi wamekosa mkopo kwa kutowasilisha baadhi ya nyaraka ingawa tuliwaomba kufanya hivyo, hawa na wengine wenye sababu za msingi, watapata fursa ya kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao na nakala kuzituma kwa utaratibu tutakaoutangaza wiki inayoanza kesho,” amesema Bw. Badru.

KOSA MLILOFANYA NI KUWACHELEWESHEA MIKOPO AMBAPO WENGI WA WANAFUNZI WAMESHARIPORT NA KUANZA MASOMO HUKU WAKITARAJI KUPEWA MIKOPO........

ALAFU LEO UNAMUAMBIA HANA SIFA ZA KUPEWA MKOPO ETI KWA SABABU ZISIZO NA MASHIKO KAMA HIZO APO JUU UNAFIKIRI KITU GANI KITAENDA KUTOKEA BAADA YA TAARIFA HIZOO.. KAMA MWANZONI MLIVYOLETA UTARATIBU WENU WA MEAN TEST KUKAWA VILE...

Huku bosi wenu akishindwa kujieleza vizuri huku akijing'atang'ata eti ooo mara bodi mnafanya kazi kwa mazoea mara kama ni ivoo bora wasipewe n.k ALAFU LEO MNAKUJA NA UPUUZI MWINGINE HUO?? HAKIKA BODI MJIANDAEE MSIMU HUU ITANYESHA MVUA NA SIO RASHARASHA ZA UD TENA ,,
MTAISOMA NAMBA....
 
Kama kuna uwezekano wa kutafuta wafadhili ni bora kufanya hivyo kuliko kuskilizia serikali, wanavyuo wengi sana watapoteza muda mwingi na mielekeo yao ya maisha kwa ujumla haitokuwa salama hata kidogo. Ni mtazamo wangu tuu
 
14906960_1001119833333643_6120554555057602529_n.jpg

UKISIKIA KWAMBA MWENDOKASI BILA UMAKINI UNAUWA ..BASI
KUUWA KWENYEWE NDIO HUKU...

BODI YA MIKOPO/HESLB...

Kwa mujibu wa Bw. Badru, kundi la kwanza linajumuisha wanafunzi waombaji wa mikopo wenye uhitaji maalum kama wenye ulemavu uliothibitishwa na Waganga Wakuu wa Wilaya na yatima ambao katika maombi yao waliwasilisha nakala za vyeti vya vifo zilizothibitishwa na makamishna wa viapo.

“Kundi la pili linajumuisha waombaji wa mikopo ambao baada ya uchambuzi wa taarifa zao walizowasilisha na baada ya kulinganisha na gharama za jumla za masomo yao ya sekondari, wamebainika kuwa wana uwezo mdogo wa kugharamia masomo yao ya elimu ya juu na hivyo kuwa na uhitaji zaidi wa mikopo,” amesema Bw. Badru.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Bw. Badru ametaja kundi la tatu na la mwisho kuwa linajumuisha waombaji wa mikopo ambao wenye ufaulu wa juu katika matokeo yao ya kidato cha sita na wamechaguliwa kujiunga na fani za kipaumbele kwa taifa.

Fani hizo ni Sayansi za Tiba, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, uhandisi wa Kilimo, Mafuta na Gesi na Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
Makundi ya wanafunzi waliopata mikopo

“Hivyo basi, hadi sasa tumetoa mikopo kwa wanafunzi 20,183 wakiwemo wanafunzi yatima 4,321, wenye ulemavu 118, wanafunzi wenye uhitaji waliosomeshwa na taasisi mbalimbali katika masomo ya sekondari (87), wanafunzi wanaosoma kozi za kipaumbele 6,159 na wanafunzi wanaosoma kozi zisizo za kipaumbele lakini wanaotoka kwenye familia duni 9,498,” amefafanua Bw. Badru.

Sababu za kukosa mikopo

Katika mkutano huo, kiongozi huyo wa HESLB pia ameeleza kwa kina sababu nyingine za waombaji 27,053 ambao hawajapangiwa mikopo.
Ametaja sababu hizo kuwa ni pamoja na baadhi ya waombaji (90) kuwa na umri wa zaidi ya miaka 30, waombaji mikopo waliopata udahili kwa sifa linganishi (equivalent qualifications) na waombaji waliomaliza masomo ya kidato cha sita zaidi ya miaka mitatu iliyopita.

Kundi jingine la waombaji waliokosa mikopo katika awamu ya kwanza ni waombaji waliopata nafasi katika vyuo kwa ufaulu wa mitihani waliyofanya kama watahiniwa binafsi (Private Candidates) na waombaji ambao hawakurekebisha fomu zao za maombi ingawa waliitwa kufanya hivyo.

Nafasi ya rufaa na uhakiki wa wanafunzi wanaoendelea na masomo
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji huyo pia amewataka waombaji ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo unaotangazwa, kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao utakaofunguliwa kuanzia katikati ya wiki ijayo.

“Tunafahamu kuwa kuna baadhi ya wanafunzi wamekosa mkopo kwa kutowasilisha baadhi ya nyaraka ingawa tuliwaomba kufanya hivyo, hawa na wengine wenye sababu za msingi, watapata fursa ya kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao na nakala kuzituma kwa utaratibu tutakaoutangaza wiki inayoanza kesho,” amesema Bw. Badru.

KOSA MLILOFANYA NI KUWACHELEWESHEA MIKOPO AMBAPO WENGI WA WANAFUNZI WAMESHARIPORT NA KUANZA MASOMO HUKU WAKITARAJI KUPEWA MIKOPO........

ALAFU LEO UNAMUAMBIA HANA SIFA ZA KUPEWA MKOPO ETI KWA SABABU ZISIZO NA MASHIKO KAMA HIZO APO JUU UNAFIKIRI KITU GANI KITAENDA KUTOKEA BAADA YA TAARIFA HIZOO.. KAMA MWANZONI MLIVYOLETA UTARATIBU WENU WA MEAN TEST KUKAWA VILE...

Huku bosi wenu akishindwa kujieleza vizuri huku akijing'atang'ata eti ooo mara bodi mnafanya kazi kwa mazoea mara kama ni ivoo bora wasipewe n.k ALAFU LEO MNAKUJA NA UPUUZI MWINGINE HUO?? HAKIKA BODI MJIANDAEE MSIMU HUU ITANYESHA MVUA NA SIO RASHARASHA ZA UD TENA ,,
MTAISOMA NAMBA....

Credit to
HOME OF INTELECTUALS-UDSM,UDOM,MZUMBE,SUA,SAUT,ARU,MAKUMIRA.
Maelezo ya bwana Badru, ukiyasikiliza unaweza kusema kweli bodi ya mikopo wamejitahidi sana,ukija kwenye uhalisia na ukifanya reference za hotuba za raisi JPM, unaweza kuamsha hasira ndani ya kichwa na kuchanganyikiwa.
Kwanza ni kweli kuwa mikopo imekuja ikiwa imechelewa na wanachuo tayari wako vyuoni,hawapokelewi mpaka walipe angalau nusu ya ada. Wengi wao walitarajia kupata mikopo kama walivyokuwa wakiamini hotuba za raisi wa nchi.

Michakato wanayofanya ili kutoa mikopo,sijui kama wameifanyia analysis za kutosha kujiaminisha kuwa kuna kundi la wanachuo wenye wazazi wenye uwezo wa kulipa.

Mi hapo ndo maswali yangu yanaanzia, maana uhalisia tumeona watoto wenye wazazi wenye uwezo na watoto wamepata mikopo na wasiokuwa na uwezo hawakupata.

Sana sana wametumia shule walizosoma vijana kujua uwezo wa wazazi.
Kwa hili nawaambia hivi,kunawazazi ambao wamesomesha watoto wao English medium school kwa kuuza mashamba yao na wakati huo huo kuna wafanya biashara wenye uwezo wa juu kabisa lakini kutoa milioni zao kwa shule hawawezi hivyo watoto wamepitia shule zetu za kawaida lakini wazazi wako vizuri.

Ngoja nitoe scenario moja, kuna binti mzazi wake hana uwezo kabisa maana alimsomesha kwa shida na mtoto yuko vizuri sana, O'level alipata div one akaenda PCB shule ya serkali kaondoka na One tena.

Kapata udaktari pale UDSM lakini kapewa mkpo wa shs 27,000!!!!
Wanamwambia akate rufaa, sasa mpaka hizo process za rufaa huyu binti atakuwa anafanya nini na tayari yuko Chuo na mkopo kama kakosa vile.

Ushauri wangu kwa bodi, wangetoa mikopo kwa wote walioomba angalau wote wapewe 50% ila kwa wale wenye mahitaji na wanaosoma fani za kipa umbele wapewe 100%. Nje ya hapo walichofanya ni kuwachanganya zaidi watu.
 
Sidhani kama kuna kusoma tena hapa nimeshakataa tamaa na hivi nina wiki tatu toka chuo kifunguliwe sijaripoti nikijipa moyo mambo yatabalika kumbe ndo yanaenda yakiwa ovyoo kabsaa
 
hiii n wk y tatu nami cjaripot chuo coz y ada kama mambo yenyw ndo haya bora nirud nyumban nkalime so kwa kutunyanyasa hivi kumbuken huu tayar ushaitwa mkopo so lzm urudishwe xx kwann mnatufanyia hivi watanzania wenzen wenyw kipato cha chini.
 
Kwa kweli ishu ya mikopo ni uonevu mkubwa sana kwa vijana wetu kujikwamua kielimu, labda serikali itoe tamko, ELIMU SI MUHIMU KWA MSTAKABALI WA NCHI, kweli kama nchi tajiri kwanini tusiwaendeleze vijana ili waje kuutumikia vyema utajiri huo? Je, vipaumbele vinabadilika baada ya watu kufika chuo? Je, bodi hawakujiandaa? Verry disappointed na hizi figisufigisu
 
Mwakani nitakuwa na miaka 30...

Ndo najiandikia hivyo kuwa Historia ya Elimu yangu itakuwa ni Diploma ambayo Ajira yake imekuwa ya kusua sua sana.

Nisipopata mkopo sijiui ila nitaungana na Ritz1 kula ganja.
 
Kipaumbele cha kwanza ni ELIMU, ELIMU, ELIMU. itakuwa bure siyo tu shule ya msingi mpaka chuo kikuu.
 
mikopo siku izi wanapewa wenye nazo yan watoto wa vigogo sisi maskini tutajijua maana daah ukiangalia watu waliopewa mkopo na walioachwa unaweza kucheka yan anyway ndo TANZANIA nchi inayo yumbishwa na watu wachache sana MUNGU ibariki nchi yangu
 
Mwakani nitakuwa na miaka 30...

Ndo najiandikia hivyo kuwa Historia ya Elimu yangu itakuwa ni Diploma ambayo Ajira yake imekuwa ya kusua sua sana.

Nisipopata mkopo sijiui ila nitaungana na Ritz1 kula ganja.
Daaah Diploma wametukazia
 
Kila awamu na mipango yake ya utoaji mikopo.
Itafika wakati mikopo itatolewa kwa.vigezo vya ukanda!
 



Hapo ni majina ya wanufaika mkopo Mzumbe.

Kozi ambazo si Kipaumbele wamepigwa 100%

Kipaumbele wengi tumetoswa.

Guidebook ya HESLB kuna mahali wameandika

"isitokee Cluster I na II wamekosa mkopo halafu wengine wapate"

Hili Bodi mmechemsha
Mungu anawaona kwa kukatiza ndoto yangu.
 



Hapo ni majina ya wanufaika mkopo Mzumbe.

Kozi ambazo si Kipaumbele wamepigwa 100%

Kipaumbele wengi tumetoswa.

Guidebook ya HESLB kuna mahali wameandika

"isitokee Cluster I na II wamekosa mkopo halafu wengine wapate"

Hili Bodi mmechemsha
Mungu anawaona kwa kukatiza ndoto yangu.
 
hiii n wk y tatu nami cjaripot chuo coz y ada kama mambo yenyw ndo haya bora nirud nyumban nkalime so kwa kutunyanyasa hivi kumbuken huu tayar ushaitwa mkopo so lzm urudishwe xx kwann mnatufanyia hivi watanzania wenzen wenyw kipato cha chini.
inauma saana inafikia kipindi unawazaa mpk unakosa majibu unaishia kujuta tu kuzaliwa tz
 
Cjui nchi inaenda wap lakn kwa swala LA mkopo dis is a seriaz issue Iv kwel we unasema n Wa watu maskin ilihali uwez onyesha kwa vitendo hapana kla mzazi alikuwa anajinyima ilihali mtoto wake fikee chuo nanajua. Atatua mzgo Wa elimu ila Leo unasema "mkopo n kwa watu maskin na wavpaumbele " maskini yup unampa wakat maskin ndo Hawa wanaolalamika wamekosa.
To a sababu y Wa equvalte uwap mkopo ..mnatupeleka peleka tuuu kama mtoto mdogo anaendesha ringi ......
...
 
Back
Top Bottom