Bodaboda anusurika kuchomwa moto

Bodaboda anusurika kuchomwa moto

Mmanu

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2015
Posts
1,977
Reaction score
1,219
Ni tukio la bodaboda alinusurika kuchomwa moto katika eneo la Sinza Afrikasana baada ya kujaribu kupora mkoba wa mwanamke aliyekuwa anatembea kwa mguu.

Baada ya kupora pikipiki yake iligoma kuwaka na ndipo wananchi walipomvamia na kuanza kumshushia kipigo. Wakati kipigo kikiendelea huku wengine wakiwa wameenda kuchukua petrol alifika trafiki katika eneo hilo na kupelekea kunusurika kijana huyo. Hat a hvyo kutokana na hasira walizokuwa nazo wananchi waliivamia pikipiki yake na kuamua kuichoma moto.
 

Attachments

  • 1427792497433.jpg
    1427792497433.jpg
    31.9 KB · Views: 681
Wamefanya maamuzi mazuri kumalizana na pikipiki japo halikuwa lengo lao,hawa vijana wamezidi.
 
Ingekuwa mafisadi nao wanafanyiwa hivyo ingekuwa jambo la maana sana.
 
safi sn wananchi wenye hasira si ajabu hata hiyo pikipiki niyawizi.
 
Huyo jamaa aliyenusurika atashtakiwa kwa wizi? nahisi ndo yameishia hapo
 
Wamefanya maamuzi mazuri kumalizana na pikipiki japo halikuwa lengo lao,hawa vijana wamezidi.
Maamuzi mabaya sana hayo...pikipiki inaweza ikawa si yake kwamba atakuwa kaajiriwa tu..sasa imagine wewe ndo mwenye pikipiki then inachomwa MOTO na ndo tegemeo lako hapo na usikute ni ya mkopo SACCOS au bank.INAUMIZA bora wangemalizana naye kwa huo huo moto.
 
Maamuzi mabaya sana hayo...pikipiki inaweza ikawa si yake kwamba atakuwa kaajiriwa tu..sasa imagine wewe ndo mwenye pikipiki then inachomwa MOTO na ndo tegemeo lako hapo na usikute ni ya mkopo SACCOS au bank.INAUMIZA bora wangemalizana naye kwa huo huo moto.

Uko sawa mkuu ila kumbuka huyo mwizi pia anaweza kuwa na familia inayomtegemea je wangemuua si wangeongeza wazururaji mtaani?kwa kuchomwa pikipiki kunawanya bodaboda wengine kuepuka na kuogopa kupora pora hovyo pia kwa mtu mwenye chombo chake akisikia bodaboda wana tabia kama hizi atajitahidi kutafuta kijana mtulivu na kabla hajamkabidhi apitie njia zote,mf:kuwa na wadhamini wanaoleweka,kukabidhiana chombo mbele ya wanasheria na vitu kama hivyo.mkuu the Hammer
sometime duniani inatakiwa litokee kosa ili kutokana na kosa sisi wengine tujifunze.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom