platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,548
- 11,517
Najua wakuu wa Vyama hivi wanatembelea JF. Na tunajua teknolojia ya habari na mawasiliano ilivyo muhimu katika kupashana habari, inaweza kuzuka hoja kwamba hii mitandao ya kijamii inatembelewa na watu wachache sana lakini jibu rahisi la hoja hiyo ni kwamba "ni kweli lakini impact yake ni kubwa sana" Juma atasoma na kumhadithia Musa ambaye hajui kutumia mtandao naye atawaeleza wenzake kule walipo . Chain ya mwasiliano itaenda kwa mfumo huo na hatimaye habari zinawafikia wengi.
Nimekuwa napitia mara mojamoja kwenye Blog ya vyama hivi Viwili (CHADEMA na CCM). CCM kwa upande wake wana blog nzuri, ina sehemu ambazo unaweza kusoma historia, katiba na miongozo yao bila kusahau Jumuiya zake.
Lakini hali ni tofauti kwa CHADEMA, ndiyo blog inaonyesha picha za harakati mbalimbali za kisiasa, matukio muhimu pamoja na picha za viongozi wake lakini inakosa vitu vingine vya ziada na muhimu sana kama Katiba, Vision, matamko muhimu ya viongozi , Ilani za uchaguzi zilizopita, hotuba n.k. Ndiyo kuna link ya wavuti lakini ni vyema hayo yote yakawepo kwenye blog pia ambayo ni rahisi kufikika
Ni muhimu kukumbuka kuwa kuna vijana wengi sana wanaingia kwenye mitandao na ni vyema wakapata fursa ya kusoma mambo ya msingi ya kichama ili wawe na mtizamo unaoleweka na pengine "kuwaambukiza" wenzao. Mimi si mwanachama wa chama chochote kile, lakini pengine kwa maoni haya watarekebisha.
Karibuni.
Nimekuwa napitia mara mojamoja kwenye Blog ya vyama hivi Viwili (CHADEMA na CCM). CCM kwa upande wake wana blog nzuri, ina sehemu ambazo unaweza kusoma historia, katiba na miongozo yao bila kusahau Jumuiya zake.
Lakini hali ni tofauti kwa CHADEMA, ndiyo blog inaonyesha picha za harakati mbalimbali za kisiasa, matukio muhimu pamoja na picha za viongozi wake lakini inakosa vitu vingine vya ziada na muhimu sana kama Katiba, Vision, matamko muhimu ya viongozi , Ilani za uchaguzi zilizopita, hotuba n.k. Ndiyo kuna link ya wavuti lakini ni vyema hayo yote yakawepo kwenye blog pia ambayo ni rahisi kufikika
Ni muhimu kukumbuka kuwa kuna vijana wengi sana wanaingia kwenye mitandao na ni vyema wakapata fursa ya kusoma mambo ya msingi ya kichama ili wawe na mtizamo unaoleweka na pengine "kuwaambukiza" wenzao. Mimi si mwanachama wa chama chochote kile, lakini pengine kwa maoni haya watarekebisha.
Karibuni.