Bifu la Shigongo na meneja wa WCB

Dumelo

Senior Member
Apr 23, 2015
139
235
Kwanza nianze kwa kusema kuwa Mimi si Fani wa DIAMOND Isipokua napenda Muziki Mzuri anaofanya, Pamoja na Jitihada, Bidii na Discipline aliyonayo katika kufanya kazi zake. Sitaki kuingia kwenye Ugomvi au Maneno au Ushauri ambao Kaka yangu Eric Shigongo ameutoa kwa Managers wa Diamond.

Hoja yangu mm ni kwamba ni Lazima tukubali kuwa Diamond amefika hapo alipo kutokana na Jitihada, Kipaji, Uchu wa mafanikio pamoja na Discipline ya Muziki wake. Swala alilotoa Le Mutuz kuwa Babu Tale na Sallam ndo Mameneja Bora wa Wasanii hapa Bongo, ni uwongo mkubwa, kwani Ili hawa mameneja wa Diamond waonekane ni mameneja Bora, ni Lazima tuone uwiano sawa wa mafanikio ya kumziki kwa wasanii wengine ambao pia wako chini yao, mfano Tiptop, Chege, Temba, Yamoto, Madee, na Tunda.

Ukiangalia hawa wasanii wamepotea kabisa kwenye game, hawana muelekeo mzuri kimziki, hawana mafanikio aliyonayo Diamond, hawafanyi show kama anazofanya Diamond, ndani na nje. Je, swali la kujiuliza ni kwamba kwann kama wao ni mameneja wazuri kwann wameshindwa kuwaweka juu kimziki hao wasanii? Je hawana kipaji kama diamond?

Je, kwanini tusikubali kwamba, kwa vile Diamond kwa kipaji chake, jitihada na Discipline aliyonayo ndo.imewavutia hawa mameneja? na hivi sasa Nguvu, akili na macho yao yote wameangalia kwa diamond maana wanajua diamond ni bidhaa au Brand inayojiuza kwa Sasa na hata bila wao bado angeweza kujiuza tu.

Kuna wakati hao walijiona wao ndo wameshika mziki wa Bongo, lakini ukweli ni kwamba wapo kwa Diamond kimasilahi, siku diamond akichuja watamkimbia tu. Hilo ndilo tatizo la kuwa na managers ambao hawajaenda shule, full Uswahili.
 
Alikiba ana kipaji na pia ana meneja walioenda shule je yupo mbali kimaisha?anamiliki nyumba ngapi?

Meneja wa kwanza wa dai alikua bob juniour kisha akaja kwa babutale na salaam waliomfikisha hapo alipo. Je mlitaka abaki kwa bob juniour au aende kwa meneja gani?

Watanzania bana ukiwa na hela linawakereketa kweli ukifulia wanafurahi na sherehe wanaandaa.
 
Shigongo anazingua sana kawachanganya bongo movies wameangukia pua, sasa hivi anawaanza wasanii wenye bifu LA kimaslahi, kama anataka hiyo percentage kama waliyoelewana na harmonize ni heri wayamalize kimyakimya tu sio kuharibiana
 
Hilo la shigongo naliacha.Hapo uliposema kwanini wasanii wengine wako chini ya diamond kimafanikio wakati meneja sawa nina swali.Lecture akiwa mzur ndo ufaulu wa wanafunzi wote utakua mzur?..ikiwa hapana je ina maana lecture atakua mbovu kwa sababu ya kufaeli kwa wachache?ikiwa ni ndio, kufaulu kwao kutakua sababu ya lecture pekee kua mzuri?
 
Kwanza mkae mkijua meneja hamfanyi msanii kuwa bora, msanii mwenyewe juhudi zake humfanya kuwa bora na duniani hamna meneja anayependa kufanya biashara isiyo na faida, hv leo kuanguka kwa Bob Valentino na Chingy utamlaum Ludacris eti,kwa hiyo usimlaumu babutale kwakufeli kwa MB dog, PNC nk. Acheni ujinga ktk maisha hamna kitu kizuri kama kujitambua unataka nini, diamond platnumz anajua anataka nini na mkae mkijua diamond platnumz alikuwa anatoza ela ndefu hata kabla ya kuwa chini ya babutale wala sallam, kwa hata ilo dau naamini diamond ndiye aliyeliweka. Hata darasani Kuna kuwa na wanafunzi wengi lakini Kuna mmoja lazima atakuwa na uwezo wapekee, kwani wote hawawezi kuwa sawa, huwezi kofosi diamond awe sawa na yamotto, chege, temba nk, kwani kila mtu ana uwezo wake. Diamond kabla ya kuwa na babutale pamoja na sallam, alikuwa chini ya papaa misifa, Raquel badae ndio akawaomba babutale na sallam wammeneji. Kuhusu mameneja kumkimbia, mimi si shangai, kama biashara hamna kila mtu akafanye shughuli nyingine na ndio maana diamond anatoza ela ndefu , anajua siku akidondoka tayari kashapiga ela anakaa pembeni anaangalia vitega uchumi vyake. Wabongo mna maneno mengi hebu niambieni hao wasanii wengine ambao wana mameneja, je wataendelea kuwa meneji milele na milele, siku zote za maisha yao, naomba kama yupo meneja ambaye ata meneji wasanii milele bila kuangalia kama anapata faida (juma nature alikuwa chini ya P Funk, je leo nature yupo chini ya P Funk), kama yupo huyo meneja, atakae mmeneji msanii siku zote, nitajieni huyo meneja na msanii wake. Mwacheni dogo apige ela ndio muda wake huu na yy Shigongo ache kuponda wenzake baada ya kuona kitumbua chake kimeingia mchanganyiko, kama anataka faida kubwa atoe ela kubwa ili apate faida kubwa. Alafu nae Shigongo nimegundua hana busara, jana ktk kipindi cha SHILAWADU, alikuwa anamtishia babutale kwa kumtangazia vita, sasa yote ya nini au anajiona yy kwasababu anamiliki magazeti, anajua atayatumia (manake waandishi wahabari wengi wanatekeleza matakwa ya maboss wao) ili kumchafua diamond platnumz atakavyo, aache tabia zake kama za mkuu wa mkoa .
 
Wanalazimisha ni comment wanavyotaka wao. Nami sipendi kuwa bendera fata upepo.
Haha ha ha ha umewafanya nini Numbisa hawa watu. huyu wa pili sasa naona anakuandama.

usipanic ivyo bana wasamehe bure maana UKIONA WANAKUFUATA UJUE UNA MAISHA MAZURI KULIKO WAO.
 
Ni baadhi ya Watanzania ndiyo wenye roho mbaya kuona Mtanzania mwenzao kafanikiwa kimaisha. Wapo wengi wanafurahi tena wanaweza hata kukupa pongezi kwa mafanikio yako. Cheza nao mbali kabisa wale wenye roho za korosho (ntima nyongo) ukishawajua.

Alikiba ana kipaji na pia ana meneja walioenda shule je yupo mbali kimaisha?anamiliki nyumba ngapi?

Meneja wa kwanza wa dai alikua bob juniour kisha akaja kwa babutale na salaam waliomfikisha hapo alipo. Je mlitaka abaki kwa bob juniour au aende kwa meneja gani?

Watanzania bana ukiwa na hela linawakereketa kweli ukifulia wanafurahi na sherehe wanaandaa.
 
Back
Top Bottom