HFOOO
JF-Expert Member
- Aug 6, 2018
- 683
- 652
Habarini wazee humu Jf
Naomba kwenda kwenye mada tajwa hapo juu, wakuu nimekuja kwenu kama kijana ambae natamani nami kutafuta kujikwamua na wimbi la umaskini na angalau kupata akiba kwa ajili ya vizazi pia.
Nimepata wazo la kuanzisha mtandao wa kibiashara kama Amazon, Alibaba, Aliexpress na Ebay, kulingana na vile ambavyo nimejifunza mengi sana kwa hizi tovuti nini wanafanya na kwa nini wamefanikiwa na kuaminiwa, na pia nimejaribu kufuatilia hizi tovuti za hapa bongo na kujua nini mapungufu yao na wapi wamekosea na mimi nataka kuongeza kitu gani ambacho wao hawana.
Nimekuja kwenu wanajamvi nikiamini humu kuna wataalamu wa kila aina na wanaoweza kutoa ushauri mzuri hasa nini natakiwa kufanya na nianze na nini katika kufikia hatua hiyo.
Katika mawazo yangu ambayo nimeona nitafanya mabadiliko kidogo kutofautisha na tovuti za hapa nyumbani ni kama ifuatavyo:
1. Ni kuwalinda watu hawa wawili wasitapeliane ambao ni mnunuzi na muuzaji,
2. kuweka mawakala kila mkoa au wilaya kadri nitakavyokuwa nimepanuka kibiashara ili mizigo inatoka kwa muuzaji ikaguliwe na kupewa namba ya mzigo na packing nzuri ,
3. Kuhakikisha team tendaji kuwa active kuwajibu wateja wetu masaa 24 wakiachiana zamu
4. Kuhakikisha mzigo wa mteja umemfikia mnunuzi ndipo muuzaji anapewa hela zake,
5. Kuhakikisha watakaopost vitu vyao ambao watataka watumiwe fedha direct na wanunuzi ni kuwafuta katika orodha ya bidhaa,
6. Kuhakikisha wateja wote mfano muuzaji yupo Mwanza na mnunuzi yupo Mwanza ni lazima mzigo uende kwa wakala wetu kwanza ndipo mnunuzi aje upokee hapo.
Hayo ndio mawazo yangu ambayo nimeona mitandao mingine hapa nyumbani hawajafanya kama hivi, Wanajamvi kwa wote kwa pamoja naombeni mwenye wazo jingine pia kuchangia na kuniongezea elimu kwa kazi hii ambayo ipo jikoni kwa sasa na week chache zijazo nitawawekea tamplate yake hapa muone na kunikosoa pale nilipokosea na kuniongezea ujuzi zaidi na pia itasaidia kutoa ajira kwa watanzania wenzangu.
Natanguliza shukrani zangu za dhati naimani wa IT mpo humu naomba mawazo yenu na wataalamu wa biashara mpo humu, na mnaofanya kazi bank pia ushauri wenu nitawezaje kupokea hela za wateja na kuwapa wateja pia,
Ujumbe: Hali ngumu kitaa ndio unaofanya watu tuchemshe akili.
Naomba kwenda kwenye mada tajwa hapo juu, wakuu nimekuja kwenu kama kijana ambae natamani nami kutafuta kujikwamua na wimbi la umaskini na angalau kupata akiba kwa ajili ya vizazi pia.
Nimepata wazo la kuanzisha mtandao wa kibiashara kama Amazon, Alibaba, Aliexpress na Ebay, kulingana na vile ambavyo nimejifunza mengi sana kwa hizi tovuti nini wanafanya na kwa nini wamefanikiwa na kuaminiwa, na pia nimejaribu kufuatilia hizi tovuti za hapa bongo na kujua nini mapungufu yao na wapi wamekosea na mimi nataka kuongeza kitu gani ambacho wao hawana.
Nimekuja kwenu wanajamvi nikiamini humu kuna wataalamu wa kila aina na wanaoweza kutoa ushauri mzuri hasa nini natakiwa kufanya na nianze na nini katika kufikia hatua hiyo.
Katika mawazo yangu ambayo nimeona nitafanya mabadiliko kidogo kutofautisha na tovuti za hapa nyumbani ni kama ifuatavyo:
1. Ni kuwalinda watu hawa wawili wasitapeliane ambao ni mnunuzi na muuzaji,
2. kuweka mawakala kila mkoa au wilaya kadri nitakavyokuwa nimepanuka kibiashara ili mizigo inatoka kwa muuzaji ikaguliwe na kupewa namba ya mzigo na packing nzuri ,
3. Kuhakikisha team tendaji kuwa active kuwajibu wateja wetu masaa 24 wakiachiana zamu
4. Kuhakikisha mzigo wa mteja umemfikia mnunuzi ndipo muuzaji anapewa hela zake,
5. Kuhakikisha watakaopost vitu vyao ambao watataka watumiwe fedha direct na wanunuzi ni kuwafuta katika orodha ya bidhaa,
6. Kuhakikisha wateja wote mfano muuzaji yupo Mwanza na mnunuzi yupo Mwanza ni lazima mzigo uende kwa wakala wetu kwanza ndipo mnunuzi aje upokee hapo.
Hayo ndio mawazo yangu ambayo nimeona mitandao mingine hapa nyumbani hawajafanya kama hivi, Wanajamvi kwa wote kwa pamoja naombeni mwenye wazo jingine pia kuchangia na kuniongezea elimu kwa kazi hii ambayo ipo jikoni kwa sasa na week chache zijazo nitawawekea tamplate yake hapa muone na kunikosoa pale nilipokosea na kuniongezea ujuzi zaidi na pia itasaidia kutoa ajira kwa watanzania wenzangu.
Natanguliza shukrani zangu za dhati naimani wa IT mpo humu naomba mawazo yenu na wataalamu wa biashara mpo humu, na mnaofanya kazi bank pia ushauri wenu nitawezaje kupokea hela za wateja na kuwapa wateja pia,
Ujumbe: Hali ngumu kitaa ndio unaofanya watu tuchemshe akili.