Benki ya Posta na Ajira za Upendeleo

Masulupwete

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
2,366
Reaction score
2,435

Mytake: Serikali inapaswa kuwa makini na namna taasisi mbalimbali zinavyoajiri watu wake. Binafsi nilipata fursa chache kuomba nafasi zinazotangazwa na benki ya posta. Kwenye matangazo yao wanasisitiza lazima maombi yatumwe kwa mtandao kwenda kwenye email yao! lakini kwa mshangao kila nikituma maombi, system inaniambia hiyo email haipo na kwamba maombi hayajaenda nikapiga simu ikapokelewa na receptionist ambae licha ya kumtaka anielekeze niongee na HR au IT manager yeye alikomaa nimweleze tatizo langu. Nikaona isiwe tabu, baada ya kumweleza tatizo yeye akanijibu eti huwa wanapata hayo maombi yanayotumwa na waombaji mbalimbali (licha ya mimi kupata return email kuwa application haijaenda!). So kuna tatizo kubwa kwenye ajira za hawa jamaa. Nawapongeza ofisi ya CAG kwa kuwabaini.

Source:Mwananchi
 
hii benk ifungwe tu kwani ni moja ya mashirika yanayoiingizia serekali hasara kila mwaka
 
haaaa dawa yao n kukopa nqkusepa bank wakisema watoke mbele nao watatoka kwan! duhhhh
 
Inakuwaje bado kuna ubabaishaji huu wakati tuliaminishwa benk imepata menejiment mpya
 
Sasa hata kama ni matatizo,hayo ni vitatizo vidogo na ungeleta mezani kwetu tungeshughulikia.Kwa kuwa umeleta kwenye mtandao wa kijamii (tena tishio) Hivyo basi kwa niaba ya menejimenti ya TPB hatutatoa nafasi ya kazi kwa wote wenye majina yanayo anza na "M" na tunaanza na wewe masulupwete.


Popote toa kitu,upate kitu!

Msemaji.
 
ha ha ha ha ha ha du tanzania bana ni zaidi ya ujijuavyo aisee
 
hawa posta bank si juzi tu wametangaza nafasi za kazi lakini ukituma maombi kwenye email yao inakataa. Kweli mafisadi
 


Haa haa haa huwez kuwa siriaz!
 
Hata mimi ni mhanga niliyejeruhiwa na masuala ya ajira kwa benki hii ya posta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…