Halafu unajua kuwa Nguo za pamba ndiyo zenye bei ghali zaidi. Shati la pamba jipya si chini ya 40,000/= Tshs. Halafu kilo moja ya pamba inatoa mashati zaidi ya mawili. Angalia sasa!!!Naomba kilio hiki kifike mamlaka husika.
Mwaka juzi kilo ya pamba tuliuza kwa 1200
Mwaka jana tuliuza kwa 1100
Mwaka huu bei elekezi ni 1200.
Naomba mtambue kuwa msimu ulikuwa mbaya sana.
Hapakuwa na mavuno kwa upande wa mazao ya kilimo kutokana na kukosekana mvua.
Ndiposa tukalima kwa wingi pamba kama zao la biashara la kutukomboa kwa kuwa linavumilia sana ukame. Lakini ukame nao ulizidi hadi na lenyewe likashindikana.
Shamba la kutoa tani 1 limetoa kilo 300 tu.
Naomba angalau bei iwe 2,000 kwa kilo
Hahaha uzuri wana sehemu ya kujifunzaNi vizuri mkachukua hata hicho kidogo,kuna wenzenu huku wameshapata magonjwa ya moyo na kisukari na wengine tumeshazika sababu ya kupigwa za uso kwenye korosho.
lHalafu unajua kuwa Nguo za pamba ndiyo zenye bei ghali zaidi. Shati la pamba jipya si chini ya 40,000/= Tshs. Halafu kilo moja ya pamba inatoa mashati zaidi ya mawili. Angalia sasa!!!