Arnold Ringo
JF-Expert Member
- Jan 23, 2014
- 2,318
- 394
Viongozi 16 wa mashina na matawi ya CCM jimbo la Ukonga wamejiengua kwenye chama hicho na kujiunga na CHADEMA jana Jumapili kwenye mkutano wa hadhara ulihutubiwa na Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi.
Viongozi hao wamesema wameamua kujiondoa kwenye chama hicho kwa kuwa ndani ya CCM hakuna ubinadamu, utu na uwajibikaji wa kweli na ndio maana nchi inaendelea kuwa masikini.
Wameeleza kuwa wamejitoa CCM na kujiunga na CHADEMA kwa kuwa ndio chama che ye dhamira ya kweli ya kupigania maslahi ya mtanzania wa leo tofauti na CCM ambayo wizi wa mali za umma ndio umtemalaki.
Akiwakabidhi kadi za CHADEMA, Katibu Mkuu wa BAVICHA Ndugu Munishi amewataka wanachama hao wapya kushirikiana ipasavyo na wanachama wenzao ili kufagia uozo wa serikali ya CCM kwenye mitaa, kata na jimbo la ukonga na hatimaye kuhakikisha CHADEMA inashika hatamu ndani ya jimbo hilo na kusukuma gurudumu la maendeleo mbele.
Viongozi hao wamesema wameamua kujiondoa kwenye chama hicho kwa kuwa ndani ya CCM hakuna ubinadamu, utu na uwajibikaji wa kweli na ndio maana nchi inaendelea kuwa masikini.
Wameeleza kuwa wamejitoa CCM na kujiunga na CHADEMA kwa kuwa ndio chama che ye dhamira ya kweli ya kupigania maslahi ya mtanzania wa leo tofauti na CCM ambayo wizi wa mali za umma ndio umtemalaki.
Akiwakabidhi kadi za CHADEMA, Katibu Mkuu wa BAVICHA Ndugu Munishi amewataka wanachama hao wapya kushirikiana ipasavyo na wanachama wenzao ili kufagia uozo wa serikali ya CCM kwenye mitaa, kata na jimbo la ukonga na hatimaye kuhakikisha CHADEMA inashika hatamu ndani ya jimbo hilo na kusukuma gurudumu la maendeleo mbele.