Basi kampuni ya Mallesa lagongana uso kwa uso na lori, wawili wafariki dunia

Basi kampuni ya Mallesa lagongana uso kwa uso na lori, wawili wafariki dunia

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Watu wawili wamefariki dunia baada ya basi la Kampuni ya Mallesa walilokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda mkoani Geita kugongana na lori la mizigo katika Kijiji cha Rumasa, Wilaya ya Chato mkoani Geita.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Geita, Safia Jongo, amezungumza na TBC Digital kwa njia ya simu na kuthibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema imetokea majira ya saa saba usiku wa kuamkia leo, Oktoba 7, 2025.

Lori la mizigo lililogongana na basi hilo lilikuwa limebeba vifaa vya ujenzi na lilikuwa likisafiri kutoka mkoani Mwanza kuelekea wilayani Kibondo mkoani Kigoma.
1759820524578.png
1759820571259.png
 
Back
Top Bottom