KERO Barabara ya Nyegezi-Mwanza Mjini ni mbovu mno, pia daraja ni dogo na Mkandarasi amelitelekeza tangu Januari 2025

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

matorola

New Member
Joined
Jul 3, 2024
Posts
3
Reaction score
0
Barabara ya Mwanza Mjini mpaka Nyegezi imekuwa ni kero kwa muda mrefu kiukweli kwa wakazi wa Mwanza na wengine wanaopita kuitumia.

Hii barabara ni mbovu inasababisha foleni hasa maeneo ya Mkuyuni, hili limechangiwa sana na Mkandarasi JASCO ambae tangu Januari 2025 alimwaga kifusi kwa ajili ya marekebisho ya barabara hiyo lakini hakuna kinachoendelea, imeachwa hadi leo.

Daraja la Mkuyuni ambalo lipo katika barabara hiyo nalo ni dogo, haliwezi kuhimili maji hasa wakati wa mvua.

Viongozi wetu wapo na wanaangalia tu kinachoendelea, nafikiri ni kwa sababu wao wakipita wanapigiwa ving'ora, so hawajali adha ambayo Wananchi tunakutana nazo.

Kiukweli ndugu wana JF tusaidiedi tunateseka.




Na hii ndo barabara kuu ya Mwanza Dar


Kiukweli bara Bara hii haifai
 
Tumeipenda wenyewee

Chaguo letu mileleee

Na wavimbe wapasuke


Hapo sasaaa, nadhani tumeimba wote
 
Haya mambo magumu sana! Barabara kuu ya kuingia kwenye jiji kubwa namna hii siyo ya Muhimu ila ya kutoka Mbagala kwenda Mbande ndo muhimu sana!
Kwa vile mwaka wa uchaguzi watakuja Mwanza kudanganya wananchi muwape kura!
 
Ndipo
Haya mambo magumu sana! Barabara kuu ya kuingia kwenye jiji kubwa namna hii siyo ya Muhimu ila ya kutoka Mbagala kwenda Mbande ndo muhimu sana!
Kwa vile mwaka wa uchaguzi watakuja Mwanza kudanganya wananchi muwape kura!
watakapotwambia mama anaupiga mwingi,
Wacha Bara Bara hata Maji kwenye baadhi ya maeneo kama Buhongwa, Nyashishi machinjioni ni shida, yanatoka mara 2 Kwa week
 
Kwa Sasa iyo Barabara imekuwa ni changamoto kubwa sana, kiasi kwamba Kuna mashimo mengi pamoja na Rasta /mbavu za mbwa zinatuaribia magari.
Lakini pia kwa ubovu uwo inasabisha foleni kubwa sana hasa nyakati za asubuhi na jioni.
Mamlaka ya Mkoa /Tanroda tunaomba mtusikilize hata mkwangue tu yahani greda lipite then boza la maji lipite.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…