Bank crdb huduma ya kupurchase mtandaoni boresheni

Bank crdb huduma ya kupurchase mtandaoni boresheni

Mapensho star

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2016
Posts
3,054
Reaction score
4,116
Habari wadau natumaini ni wazima
Nianze moja kwa moja na mada kama kichwa cha habari hapo juu
kadiri siku zinavyokwenda na watumiaji wa mitandao wanaongezeka lakini hawa wenzangu bank ya crdb naona wapo nyuma kidogo kuboresha huduma zao za kupurchase mtandaoni nachosema na hata ukipitia uzi mbalimbali humu utakubalina na mimi
moja ya matatizo niliyokutana nayo muda mrefu mpaka sasa hayafanyiwi kazi haya hapa
1.ukilipia pesa kwa paypal ile pesa haikatwi muda huo yani bank hawaruhusu itoke kwa wakati hivyo unakuwa unashindwa kuelewa pesa iliyokatwa ni kiasi gani na iliyobaki ni kiasi gani sababu ukiangalia salio unakuta bado lipo vile vile
2.unaweza kuwa na salio kwenye account lakini ukitaka kufanya malipo mtandaoni inashindikana kunakuwa na usumbufu mara ufike tawi letu kwa msaada na hii huwa ni mara kwa mara
3.mimi card ya crdb nilikuwa naitumia tu kufanya malipo online sasa kama card haina kitu ukitaka kununua bidhaa inabidi tena uwe na ile elfu ya kumi ya inayotakiwa kubakia kwenye account nilishawahi kukutana na hii kitu nataka ninunue bidhaa ya bei dolla 50 nakuta naambiwa sijui salio halitoshi inabidi elfu kumi ibakie kwenye account sasa nikawa najiuliza inamana malipo niliyofanya mara ya kwanza ndo wakakata hadi pesa inayobakia kweny account niliishia kuboreka tu siku ile
Ushauri wangu tu mngekuwa na card yakufanya malipo tu mtandaoni mana naona kama inakuwa usumbufu
Mana leo tena nilikuwa nataka ninunue kitu nimeweka kabisa salio la malipo nalotaka kulipia huduma mtandaon naona tena inakuwa declined nawauliza wanaishia tu kuniambia ongeza hela bila maelezo mengine
Nikaona isiwe tabu nikalipia kwa bank abc kupitia mpesa master card ambao wapo fasta bila longo longo na kiasi wanachokuwa wanakata wanakwambia kabisa
 
CRDB naona hawapo sawa katika hili.Hata customer care nako ni shida.Ukiuliza,ama wana maelezo ya juu juu au wepesi sana kukuambia uende kwenye tawi - very unprofessional.

Huwa mpaka najiuliza,labda wana ka-kampeni ka kuona wateja wanaingia benki physically kwa idadi fulani kila siku kwenye matawi, hivyo kulazimika kuzalisha mikwamo na kadhia ili wateja muende matawini-sijui mifumo ya mitandao ni migeni na inawatia mno kinyaa kiasi ya kama inawanyang'anya utamu na uhuru wa kukutana na wateja kila mara?

Binafsi wananiboa mno.Ni kama ni mtambo wa kukera tu wateja.
 
CRDB kitengo cha customer experience & care ndio hovyo kabisa sijui KPI za hao wafanyakazi wao ni nini hasa. Wanachojua ni kukujibu tatizo lako tumelipokea na tunalishughulikia, changamoto yao kubwa ukiripoti tatizo au kujaza fomu zao hawafatilii wala kutoa mrejesho. ni bank gani wako smart kwenye online purchasing?
 
Hata miaka mitano tangu Kimei astaafu tayari benki imeana kuporomoka?
This is the beginning of the end.
 
Nilishaitupa hata kad yenyewe ya crdb sasa hiv nipo nmb . Kwanza app yao nzuri ipo update. Cedb siwapend wana makato san
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom