Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,488
- 16,646
Mashambulizi yanayofanywa na Marekani nchini Yemen hayajaonesha dalili yoyote ya kupunguza nguvu za wanamgambo wa Houth kuendeleza mapambo ya kuwatetea wenzao wa Palestina.
Kinyume chake wanamgambo hao wanaonekana kupata nguvu zaidi na teknolojia za kurusha makombora mpaka kaskazini ya Israel mpakani na Lebanon.
Hapo jana makombora mawili yalirushwa moja ndani ya TeleAviv na la pili kulenga kambi ya kijeshi ya Ramat David kaskazini ya taifa hilo dhalimu.
Msemaji wa Houth meja jeneral Yahya Saree amesema makombora hayo yalipiga kikamilifu maeneo lengwa.
Kwa upande wa wasemaji wa jeshi la Israel wametoa maelezo yenye utata kwa kusema kombora moja walijaribu kulitungua na la pili wanaendelea kulifanyia uchunguzi.
Katika muendelezo wa matukio hapa mashariki ya kati, waziri wa ulinzi wa Marekani Pete Hegseth amesema baada ya wiki watairudisha nyumbani meli ya kivita ya USS Harry S Truman.
Hii ndiyo ile meli ambayo wiki iliyopita ilicheza ndombolo na makombora na droni za Houth na hatimae kupoteza ndege yake moja ya kivita ya f 18 pamoja na vifaa vya kazi ndani ya meli hiyo.
Kinyume chake wanamgambo hao wanaonekana kupata nguvu zaidi na teknolojia za kurusha makombora mpaka kaskazini ya Israel mpakani na Lebanon.
Hapo jana makombora mawili yalirushwa moja ndani ya TeleAviv na la pili kulenga kambi ya kijeshi ya Ramat David kaskazini ya taifa hilo dhalimu.
Msemaji wa Houth meja jeneral Yahya Saree amesema makombora hayo yalipiga kikamilifu maeneo lengwa.
Kwa upande wa wasemaji wa jeshi la Israel wametoa maelezo yenye utata kwa kusema kombora moja walijaribu kulitungua na la pili wanaendelea kulifanyia uchunguzi.
Katika muendelezo wa matukio hapa mashariki ya kati, waziri wa ulinzi wa Marekani Pete Hegseth amesema baada ya wiki watairudisha nyumbani meli ya kivita ya USS Harry S Truman.
Hii ndiyo ile meli ambayo wiki iliyopita ilicheza ndombolo na makombora na droni za Houth na hatimae kupoteza ndege yake moja ya kivita ya f 18 pamoja na vifaa vya kazi ndani ya meli hiyo.