Averos
JF-Expert Member
- Aug 6, 2010
- 993
- 695
Ewe sheikh ndugu yangu, hii dunia ya Qawi
Utazame ulimwengu, likutakalo haliwi
Ndio kalamu ya Mungu, viumbe hatuijuwi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Bahati imegeuka, watatu hazidishiwi.
Wa moja afurahika, mbili hazimsumbui
Mkavu wanawirika, mbichi hauchipui
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Wa kisamvu ala nyama, wa samli ala tui
Simba limekuwa ndama, makucha hayapapui
Kieleacho huzama, shina limekuwa tawi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Wa kilio yuwacheka, war aha hafurahiwi
Wa nyuma wanatukuka, wanena hawarudiwa
Wa mbele wanatihika, wasema hawasikiwi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Utazame ulimwengu, likutakalo haliwi
Ndio kalamu ya Mungu, viumbe hatuijuwi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Bahati imegeuka, watatu hazidishiwi.
Wa moja afurahika, mbili hazimsumbui
Mkavu wanawirika, mbichi hauchipui
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Wa kisamvu ala nyama, wa samli ala tui
Simba limekuwa ndama, makucha hayapapui
Kieleacho huzama, shina limekuwa tawi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa
Wa kilio yuwacheka, war aha hafurahiwi
Wa nyuma wanatukuka, wanena hawarudiwa
Wa mbele wanatihika, wasema hawasikiwi
Bahati yenda kwa muwi, wema wakalia ngoa