Baba anatuchonganisha?


Kwani baba asiye na msimamo kama hili baba letu waswahili wanamuitaje kwa jina moja???? naomba jibu......
 
Baba ambaye ukoo wake umeshindwa kumwelewa maana kila wakati amekuwa akiwaambia wanandugu muwe na akili za Mbayuwayu yaani za kuambiwa changanya na zako. Baba ambaye hajui kukemea watoto wake katika ukoo.
Tatizo baba yetu huyu ni mvivu kutwa kucha anapeleka bakuli kuomba omba kama Matonya sielwi anatufundisha nini sisi wanawe huku
 



Washauri wako wengi tu wengine wa hiari na ndiyo maana anafanikiwa kila hatua!
Huoni hizi sifa zote zinazomwangukia au huoni!

Ila kikubwa anachanganya za kuambiwa na zake.

 
Baba gani huyo anaongea na watoto anakenuakenua kama mwehu afu cha kushangaza kale kadogo kake kale kakulialia kanataka kuchukua mji. Hivi wanatuonaje, atoke wa kukenuakenua aingie wa kulialia!!!!! Let us wait and see

hako kalikosemaga watoto wengine wapigwe tu maana kamechoka! kuna karafiki kake na huyu baba alisemaga hawajakutana barabarani kanataka kaachiwe mji eti, halaf kanatumia mali kalizoiba hapa ili kafanikiwe kuwa baba mwenye nyumba!
 
Umenichekesha sana kijana, kweli baba amezidi kuzurura eti kisa anatembea kapu, miaka 9 bado hachoki kutembeza bakuli? Kwanini asitulie hapa waje wao maana wameshamfahamu na wamemwelewa kuwa tunachotaka watoto ni kipi!

 
Umenichekesha sana kijana, kweli baba amezidi kuzurura eti kisa anatembea kapu, miaka 9 bado hachoki kutembeza bakuli? Kwanini asitulie hapa waje wao maana wameshamfahamu na wamemwelewa kuwa tunachotaka watoto ni kipi!

Mdogo wangu mie ni mdada ninayekaribia kuustaafu.Ujana umeshaisha mdogo wangu.Nawaonea huruma vijana wangu hawa baba wakambowasije watoa macho yenu maana wanahasira sana.Achoke na yale mahekalu wajomba watajengaje? Binamu, zetu na wapwa wamepelekwa nje kusoma wanahitaji tuition fees.Acha mdogo wangu hawezi kuacha.
 


nasikia baba huyu huyu nae akishaondoka ataitwa shujaa.hahahahah
 
Ila babu alituambia mtu huyu hafai kuwa baba lakini kwa 'njaa' za kikundi cha watoto wanajiita wana-mtandao waka kuuza ushauri wa babu na kumpa mtu huyo ubaba, kupitia mwanaye kipenzi amejimilikisha kila kizuri cha nyumba hii na kwiba kila achoweza na kuufanya 'ubaba' uonekane ni rahisi rahisi adi kuwatamanisha watoto wengi watukutu kuutamani ubaba, sasa tunakiona cha 'mtemakuni'
 
Umetisha-Lizbon kishakupata
 
Tetty ukiona baba anahongwa na wageni saa, suti etc ili wageni walale na mama yetu huku baba akisifia ufundi kwa kusema .... Ukitaka kula lazima na wewe uliwe, ujue huyo baba ana walakini, na hajui wajibu wake kama baba wa familia
 
Last edited by a moderator:
Halafu huyu faza hataki kukaa nyumbani, yeye kila wakati kiguu na njia. Faza hana akili ya kujitegemea, anadhalilisha familia kuomba omba.

Kwakweli ametupa aibu sana wanafamilia, tena akitamka kwamba asipotembeza kwato zake kwa majirani basi sisi tutakufa na njaa kweli?. ilihali tuna mashamba tena yenye rutuba kuliko kule kwa jirani, yaan amekua mvivu wa kufikiri mpaka inaboa kwakweli labda tuombe awe ni baba wa kambo siku tutamjua baba yetu halisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…