Baadhi ya Dawa za mitishamba ni hatari

"Too much of anything is humful "
Kitu chochote kikizidi kiasi kinakua sumu. Hata maji tu ukinywa kupita kiasi yanakuuwa
 
Unahukumu wote kwa kosa la mmoja je za hospital haziui figo
 
Hivi kuna mtu kashawahi kupata tiba toka kwako akaja humu kutoa ushuhuda japo kidogo tuone ulimsaidiaje maana mwisho siku atuoni mtu kila siku wasema watibu
 
Ni dawa nzuri ila tatizo ni vipimo, wauzaji hawana elimu, ni elimu ya kukariri tu.
 
Sasa hivi ongeza na madaktari wa mitamdaoni. Kisukari imekuwa ni dili na wengi wa hawa madaktari wa mchongo wanajaza matangazo yasiyokuwa na ukweli. Tahadhari kabla ya hatari.
 
Dawa za mitishamba ni nzuri ila akikuambia kunywa vijiko viwili kunywa kimoja akisema kunywa kimoja wewe kunywa nusu dawa huwa ni kali sana japo zinasaidia
 
Dawa za mitishamba ni hatari Kwa kuwa chemical composition yake haipo well known
 
Sasa wewe unakisukari na unatumia karafuu unategemea nini ndugu yangu?
 
Tiba ya kisukari ni kuhakikisha unatibia kongosho lako liweze kufanya kazi kwa ufanisi. Ilikupasa utafute tiba ya kongosho na sio kisukari.

Tiba ya mitishamba ni nzuri ila hata mimi siitumii. Maana inaweza kutibu ini na ikaharibu figo. Unaweza kutibu figo ikaharibu moyo.

Kwanza sio kila tiba iliyokubali ka huyu itafaa kwa yule.

Mimi huwa naamini kwenye kula vizuri ndo tiba ilipo. Kwa mfano inasemekana carrots zina vitamin A ambayo ni nzuri kwa macho. Basi natumia.
Kesho anakuja mtu ananiambia majani ya mpera yanatibu macho, inaanzaje kuniingia akilini? Kama nikipata tatizo naenda hospitali kwa wataalamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…