Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,371
Kama kweli tunamuogopa Mungu na ili kutenda haki, nato wito wale wato wanaotuhumiwa katika kashifa mbalimbali kama kuua/kuhujumu lilikokuwa shirika la ndege la Tanzania (ATC),vyama vya ushirika, n.k pamoja na wale waliotajwa katika ripoti za madini za hivi karibuni, wote nao wasitishiwe pension kwa waliostafu(kama wapo) na wanaotarajiwa kustaafu nao wasitishiwe mafao yao huku ambao kwa sasa ni wanasiasa wafukuzwe na ambao ni watumishi wa umma nao watimuliwe.
Kwasababu ni tuhuma, yule anaeona amronewa aende mahakamani ila serikali nayo hapo hapo imshitaki kwa uhujumu uchumi au ufisadi au matumizi mabaya ya madaraka.
Inasiktisha sana saa hizi watanzania wanabebeshwa mzigo wa kuifufua ATCL huku walioihujumu wakiwa wanadunda mtaani huku wakila pensheni zao alafu hapo hapo tunajisifu kwa kutimua watumishi waliokuwa na vyeti feki.
Inasikitisha zaidi kujisifu kuwa tumefukuza watumishi wenye vyeti feki na kuamua kutowapa hata kifuta machozi wakati waliotajwa kwenye ripoti za makiniakia na kashifa nyingine wakiendelea na ubunge wao huku waliikuwa watendaji wakiendelea kulipwa mishahara yao.
Mimi nasema hapa tumejitengenezea dhambi na pengine hata laana kwa mwenyezi Mungu kwa kuadhibu hawa wanyonge huku mapapa ya ufisadi yakiendelea kula mema ya nchi hii.
Na si hivyo tu, bali tumetengeneza kumbukumbu mbaya hata kwa vizazi vijayo na nio ombi langu kwa serikali ijayo iangalie uwezekano wa kuwapa walau kifuta machozi maana tumeshindwa kutenda haki hivyo nao wafikiriwe.
Ukiwaona hawa watu baadhi yao wanavyoteseka huku wahujumu uchumi na mafisadi wakiwa wanapeta, kwa hakika inaumiza sana.
Ipo siku na nyie mtawajibika tu.
Kwasababu ni tuhuma, yule anaeona amronewa aende mahakamani ila serikali nayo hapo hapo imshitaki kwa uhujumu uchumi au ufisadi au matumizi mabaya ya madaraka.
Inasiktisha sana saa hizi watanzania wanabebeshwa mzigo wa kuifufua ATCL huku walioihujumu wakiwa wanadunda mtaani huku wakila pensheni zao alafu hapo hapo tunajisifu kwa kutimua watumishi waliokuwa na vyeti feki.
Inasikitisha zaidi kujisifu kuwa tumefukuza watumishi wenye vyeti feki na kuamua kutowapa hata kifuta machozi wakati waliotajwa kwenye ripoti za makiniakia na kashifa nyingine wakiendelea na ubunge wao huku waliikuwa watendaji wakiendelea kulipwa mishahara yao.
Mimi nasema hapa tumejitengenezea dhambi na pengine hata laana kwa mwenyezi Mungu kwa kuadhibu hawa wanyonge huku mapapa ya ufisadi yakiendelea kula mema ya nchi hii.
Na si hivyo tu, bali tumetengeneza kumbukumbu mbaya hata kwa vizazi vijayo na nio ombi langu kwa serikali ijayo iangalie uwezekano wa kuwapa walau kifuta machozi maana tumeshindwa kutenda haki hivyo nao wafikiriwe.
Ukiwaona hawa watu baadhi yao wanavyoteseka huku wahujumu uchumi na mafisadi wakiwa wanapeta, kwa hakika inaumiza sana.
Ipo siku na nyie mtawajibika tu.