Pfizer
JF-Expert Member
- Mar 25, 2021
- 726
- 953
PART 1.
Ndugu zangu Watanzania!
Amani ya Bwana na iwe nanyi!
Ashukuriwe Mungu kwa kutuwezesha kuuona mwaka mpy kwani siyo jambo rahisi kwetu Sisi watanzania baada ya kushuhudia maelfu ya watu wakiuawa , wengine kutekwa na hawajulikani walipo, na wengine wako magerezani. sio kwamba Sisi tuliouona mwaka kuwa tumejilinda wenyewe, wala kwamba ni wema sana kuliko wengine, la hasha! Ni ni neema zake Mwenyezi Mungu tu.
Ndugu zangu Watanzania,mimi Askofu nikiwa huku Nchi ya Ugeni kwa ukimbizi ninatoa salamu hizi nikiwa nimejawa na simanzi nzito sana juu ya Taifa letu la Tanzania ambalo kwa nyakati hizi limepoteza haki, Amani na utulivu kwa watu wa tabaka la chini yaani Wananchi wa kawaida. Na hii ni kutokana na kushamiri kwa matukio mabaya yanayoharibu taswira ya Taifa letu, ikiwa ni pamoja na uvunjwaji wa haki za Binadamu kama vile utekaji na mauaji ya Raia wasio na hatia.
Ndugu zangu Watanzania hususani Tanganyika,Taifa letu limekuwa kama Nchi ya ukimbizi kwa sasa kwani licha ya kushamiri kwa matukio mengi ya utekaji na mauaji ya wakosoaji wa Serikali, lakini pia Nchi yetu tumepoteza kabisa sifa ya kuitwa Nchi ya Kidemokrasia inayofuata mfumo wa vyama vingi kama ilivyoasisiwa mwaka 1992, kwani siasa za Nchi yetu kwa sasa zinazomilikiwa na Chama kimoja, hasa CCM mtandao, huku Chama kikuu cha upinzani kikizuiliwa kufanya siasa kwa namna yoyote ile na viongozi wake kuwindwa na kutajwa kama magaidi na wahaini.
Ndugu Watanzania, mtakumbuka ya kwamba mwaka 2025 Kanisa letu la Ufufuo na Uzima ambalo mimi ni Naibu katibu mkuu wake tulifutiwa usajili kihuni na kwa uonevu makubwa pasipo kuambiwa sababu za msingi. Hii ni kutokana na msimamo wa Askofu wetu Mkuu Josephat Gwajima kukemea matukio ya utekaji hadharani ambayo yanahisiwa kufanywa na watu wenye jina la "Wasiojulikana" wanaoonekana kuwa na nguvu kuliko vyombo vya ulinzi na usalama.
Mamilioni ya waumini wetu walikosa haki yao ya msingi ya Uhuru wa Kuabudu, katika kudai haki hiyo, watu wetu zaidi ya 160 waliwekwa rumande, wengine kuvunjwa mikono, miguu na viuno na Mali za kanisa kuporwa na jeshi la Polisi. Ni mwaka ambao kwa Mara ya kwanza, watu wamezuiliwa kwenda misikitini na makanisani kumwabundu Mwenyezi Mungu kwa sababu ya lockdown wakati wa uchaguzi. Jambo ambalo halitasahaulika kwa waislamu na wakristo kwenye historia zao za Kuabudu na wala Mwenyezi Mungu hatawasamehe waliofanya hayo.
Mwaka 2025 ,matukio mengi ya utekaji yalishamiri Sana kwani nilipoteza Rafiki yangu Mdude Nyagali ambaye alitekwa Mwezi Mei akiwa nyumbani kwake kule jijini Mbeya mbele ya Mkewe na watoto wake na hivyo mpaka leo hajaweza kupatikana,Ndugu yetu Humphrey Polepole alitekwa Dar es Salaam,Ndugu yetu Amani Manengelo na wengineo wengi ambao walikuwa mstari wa mbele katika Kupigania mabadiliko ya kweli katika Taifa.
Ama hakika machozi yananidondoka kila nikiwakumhmbuka hawa Ndugu zetu hakika Mwenyezi Mungu hatakosa kulipa kisasi kwa waliohusika.
Ndugu zangu,sote tunatambua ya kwamba,mwaka 2025 ni mwaka ambao tulipatwa na msiba mzito kama Taifa kutokana na kuondokewa na Ndugu zetu maelfu waliokuwa wakitumia haki yao ya kikatiba kuandamana kupinga uchaguzi mkuu na hivyo kupigwa risasi za moto na vyombo vya usalama kuanzia Oktoba 29 mpaka 31 katika maeneo mbalimbali Nchini Tanzania na hata wengine ambao hawakuwa katika maandamano hayo!
Lakini jambo la kustaajabu ni kwamba mpaka sasa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa juu ya mauaji hayo na wala hayupo aliyewajibishwa kwa vitendo vile vya unyama.
Ndugu zangu, Nchi yetu inaongozwa na mfumo wa Kidikteta chini ya Utawala wa mama Samia ambaye alijipitisha na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pasipo ridhaa ya Wananchi wa Tanzania na ndiyo maana wanatuona Watanganyika ni kama ngoma ya kuchezea na kuimba mapambio yao ya amani kila kukicha ikiwa ni pamoja na kuwatumia machawa kuhalalisha uchafu wao walioufanya. Mfano kushambulia Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kisa walikemea utekaji na wizi wa kura,lakini pia kutuma hao machawa waje kumjibu na kumchafua Askofu Gwajima ambaye naye alikemea utekaji unaofanyika hapa Nchini!
Kundi hilo la Machawa ambao wengine ni viongozi wa Dini wameonekana kuwa mbele na kuchafua taswira kwa Waumini wao wanaoamini katika haki kwani madai ya viongozi hawa TEC,Askofu Gwajima na viongozi wa Kiislamu kama Sheikh Ponda na Masheikh wengineo ndiyo madai ya Wananchi.
Ndugu zangu Watanzania,kama nilivyowajulisha hapo mwezi Agosti mimi Askofu Mwanamapinduzi nililazimika kukimbilia uhamishoni katika Nchi ya ugeni kutokana na usalama wangu kuwa hatarini hali iliyopelekewa na misimamo yangu ya kupigania haki katika Taifa langu. Hapo ndipo walipoanza kunitafuta na nilipoamua kuchukua hatua ya kukimbia Nchi ili kuiokoa roho yangu na nisijisalimishe mikononi mwa watesi wetu kwani ndiyo njia niliyoiona ni sahihi kwangu ili nirudi kupigana tena kesho kwa mara nyingine.
Inaendelea Part 2......
ASKOFU MWANAMAPINDUZI,
1/1/2025
Ndugu zangu Watanzania!
Amani ya Bwana na iwe nanyi!
Ashukuriwe Mungu kwa kutuwezesha kuuona mwaka mpy kwani siyo jambo rahisi kwetu Sisi watanzania baada ya kushuhudia maelfu ya watu wakiuawa , wengine kutekwa na hawajulikani walipo, na wengine wako magerezani. sio kwamba Sisi tuliouona mwaka kuwa tumejilinda wenyewe, wala kwamba ni wema sana kuliko wengine, la hasha! Ni ni neema zake Mwenyezi Mungu tu.
Ndugu zangu Watanzania,mimi Askofu nikiwa huku Nchi ya Ugeni kwa ukimbizi ninatoa salamu hizi nikiwa nimejawa na simanzi nzito sana juu ya Taifa letu la Tanzania ambalo kwa nyakati hizi limepoteza haki, Amani na utulivu kwa watu wa tabaka la chini yaani Wananchi wa kawaida. Na hii ni kutokana na kushamiri kwa matukio mabaya yanayoharibu taswira ya Taifa letu, ikiwa ni pamoja na uvunjwaji wa haki za Binadamu kama vile utekaji na mauaji ya Raia wasio na hatia.
Ndugu zangu Watanzania hususani Tanganyika,Taifa letu limekuwa kama Nchi ya ukimbizi kwa sasa kwani licha ya kushamiri kwa matukio mengi ya utekaji na mauaji ya wakosoaji wa Serikali, lakini pia Nchi yetu tumepoteza kabisa sifa ya kuitwa Nchi ya Kidemokrasia inayofuata mfumo wa vyama vingi kama ilivyoasisiwa mwaka 1992, kwani siasa za Nchi yetu kwa sasa zinazomilikiwa na Chama kimoja, hasa CCM mtandao, huku Chama kikuu cha upinzani kikizuiliwa kufanya siasa kwa namna yoyote ile na viongozi wake kuwindwa na kutajwa kama magaidi na wahaini.
Ndugu Watanzania, mtakumbuka ya kwamba mwaka 2025 Kanisa letu la Ufufuo na Uzima ambalo mimi ni Naibu katibu mkuu wake tulifutiwa usajili kihuni na kwa uonevu makubwa pasipo kuambiwa sababu za msingi. Hii ni kutokana na msimamo wa Askofu wetu Mkuu Josephat Gwajima kukemea matukio ya utekaji hadharani ambayo yanahisiwa kufanywa na watu wenye jina la "Wasiojulikana" wanaoonekana kuwa na nguvu kuliko vyombo vya ulinzi na usalama.
Mamilioni ya waumini wetu walikosa haki yao ya msingi ya Uhuru wa Kuabudu, katika kudai haki hiyo, watu wetu zaidi ya 160 waliwekwa rumande, wengine kuvunjwa mikono, miguu na viuno na Mali za kanisa kuporwa na jeshi la Polisi. Ni mwaka ambao kwa Mara ya kwanza, watu wamezuiliwa kwenda misikitini na makanisani kumwabundu Mwenyezi Mungu kwa sababu ya lockdown wakati wa uchaguzi. Jambo ambalo halitasahaulika kwa waislamu na wakristo kwenye historia zao za Kuabudu na wala Mwenyezi Mungu hatawasamehe waliofanya hayo.
Mwaka 2025 ,matukio mengi ya utekaji yalishamiri Sana kwani nilipoteza Rafiki yangu Mdude Nyagali ambaye alitekwa Mwezi Mei akiwa nyumbani kwake kule jijini Mbeya mbele ya Mkewe na watoto wake na hivyo mpaka leo hajaweza kupatikana,Ndugu yetu Humphrey Polepole alitekwa Dar es Salaam,Ndugu yetu Amani Manengelo na wengineo wengi ambao walikuwa mstari wa mbele katika Kupigania mabadiliko ya kweli katika Taifa.
Ama hakika machozi yananidondoka kila nikiwakumhmbuka hawa Ndugu zetu hakika Mwenyezi Mungu hatakosa kulipa kisasi kwa waliohusika.
Ndugu zangu,sote tunatambua ya kwamba,mwaka 2025 ni mwaka ambao tulipatwa na msiba mzito kama Taifa kutokana na kuondokewa na Ndugu zetu maelfu waliokuwa wakitumia haki yao ya kikatiba kuandamana kupinga uchaguzi mkuu na hivyo kupigwa risasi za moto na vyombo vya usalama kuanzia Oktoba 29 mpaka 31 katika maeneo mbalimbali Nchini Tanzania na hata wengine ambao hawakuwa katika maandamano hayo!
Lakini jambo la kustaajabu ni kwamba mpaka sasa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa juu ya mauaji hayo na wala hayupo aliyewajibishwa kwa vitendo vile vya unyama.
Ndugu zangu, Nchi yetu inaongozwa na mfumo wa Kidikteta chini ya Utawala wa mama Samia ambaye alijipitisha na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pasipo ridhaa ya Wananchi wa Tanzania na ndiyo maana wanatuona Watanganyika ni kama ngoma ya kuchezea na kuimba mapambio yao ya amani kila kukicha ikiwa ni pamoja na kuwatumia machawa kuhalalisha uchafu wao walioufanya. Mfano kushambulia Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kisa walikemea utekaji na wizi wa kura,lakini pia kutuma hao machawa waje kumjibu na kumchafua Askofu Gwajima ambaye naye alikemea utekaji unaofanyika hapa Nchini!
Kundi hilo la Machawa ambao wengine ni viongozi wa Dini wameonekana kuwa mbele na kuchafua taswira kwa Waumini wao wanaoamini katika haki kwani madai ya viongozi hawa TEC,Askofu Gwajima na viongozi wa Kiislamu kama Sheikh Ponda na Masheikh wengineo ndiyo madai ya Wananchi.
Ndugu zangu Watanzania,kama nilivyowajulisha hapo mwezi Agosti mimi Askofu Mwanamapinduzi nililazimika kukimbilia uhamishoni katika Nchi ya ugeni kutokana na usalama wangu kuwa hatarini hali iliyopelekewa na misimamo yangu ya kupigania haki katika Taifa langu. Hapo ndipo walipoanza kunitafuta na nilipoamua kuchukua hatua ya kukimbia Nchi ili kuiokoa roho yangu na nisijisalimishe mikononi mwa watesi wetu kwani ndiyo njia niliyoiona ni sahihi kwangu ili nirudi kupigana tena kesho kwa mara nyingine.
Inaendelea Part 2......
ASKOFU MWANAMAPINDUZI,
1/1/2025