Ashukuriwe Mungu; Waziri mkuu Kassim Majaliwa arudisha matumaini mapya kwa wananchi wa Manyara

Jim007 2

JF-Expert Member
Dec 28, 2012
395
247
Hati ya Manyara Ranch yarejeshwa Kwa Wananchi.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amerejesha Ardhi ya Manyara Ranch Kwa wananchi wa vijiji wa Esilalei Na Ortukai Wilayani Monduli (acre 44,000).

Waziri Mkuu amekabidhi Hati ya umiliki wa Shamba Hilo Kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Monduli Ndg. Steven Ulaya Kwa niaba ya wananchi alipokua Akizungumza Na wananchi wa Monduli Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Mji mdogo wa Mto wa Mbu.

Alisema wakati wa wananchi umefika wa kumiliki Ardhi Yao Na kufanya shughuli zitakazowaongezea kipato kutoka kwenye Ardhi Yao.

Shamba La Manyara Ranch lilichukuliwa Na Taasisi ya TLCT ( tanzania land conservation Trust) Kwa zaidi ya miaka kumi sasa lakin hivi sasa umiliki wa Ardhi hiyo umerejeshwa Kwa wananchi.

Hongera sana Serikali ya Awamu ya Tano
Hongera Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Hongera Kwa Waziri Mkuu
HongeRa Kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha



 
Inasemakana hilo shamba lilihodhiwa na fisadi EL huko Monduli.....
AlijiZungurushia pasi ya kisigino.hii bavicha wakijua watamwagika kulaani mzee kuporwa eka 44,000 za nini zote anakaa nazo tu
 
Maigizo ya pwagu na pwaguzi.
Wahusika:-
Jpm = Pwagu
Km = Pwaguzi
 
Mbona eneo hilo ni mapito ya wanyama (wildlife corridor ) kwa hifadhi ya Taifa ya Manyara na Tarangire?Ni muhimu sana kufikiri matumizi ya eneo hilo isiharibu mapito ya wanyama pori kutoka Ngorongoro,Manyara na Tarangire.
 
Inasemakana hilo shamba lilihodhiwa na fisadi EL huko Monduli.....

Ni kweli yeye Edward lowasa ndiye alikuwa mwenyekiti wa hiyo KITU INAJIITA tanzania land conservation Trust iliyohodhi hilo eneo
 

bado kibo ESTATE YA HAPA HAI
 
Serikali hii ni mpango wa Mungu

Serikali hii ni kazi ya mikono yetu kupitia kura zetu mwaka jana. Acha kumkufuru Mungu bila sababu. Tutavuna tulichopanda. Mungu hajatupandia chochote hapo. Get the facts right....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…