Doctor Mama Amon
Platinum Member
- Mar 30, 2018
- 2,311
- 3,490
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, amesema kuwa chama cha Chadema kitaendelea na mpango wake wa kuzuia uchaguzi kwa sababu hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika kwenye mifumo ya uchaguzi ili kuifanya iwe rafiki kwa wadau wote.
Mnyika amesema haya kufutia kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa 31 Machi 2025, kuwa kuna mabadiliko makubwa yamefanyika kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.
Mnyika, aliyasema hayo wakati akiwahutubia watia nia katika nafasi za urais, ubunge na udiwani, waliokusanyika makao makuu ya Chadema Mikocheni , Dar es Salaam.
Aliwambia watia nia kwamba: Chadema tunao Wagombea, Ajenda, Mtandao wa makampena, Rasilimali, Wapiga Kura Makini, Isipokuwa Mfumo wa Uchaguzi Ulio Rafiki wa Wote.
Hivyo, Mnyika akawataka watia nia wote waungane pamoja ili kupigania fumo wa Uchaguzi ulio Rafiki kwa wadau wote, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi Mkuu wowote ujao.
Akifafanua kauli yake, Mnyika alisema kwamba, ili tuweze kushinda uchaguzi wowote tunahitaji mambo makuu sita.
Mosi, anatakiwa mgombea anayekubalika na anayeweza kunadi sera za chama;
Pili, inatakiwa ajenda inayogusa maisha ya wapiga kura, ikiwa imeandikwa kwenye ilani ya chama;
Tatu, unapaswa kwepo mtandao mpana wa makampen wanaotokana na ogananaizesheni ya chama kilichomcdhamini mgombea;
Nne, zinahitajika rasilimali zinazojumuisha vitu na fedha kwa ajili ya kuwafikia wapiga kura popote watakapokuwa,
Tano, lazima tuwe na wapiga Kura makini wenye kuelewa dhana kwamba kupiga kura ni mkakati wa kutatua matatizo ya kijamii kwa kufananisha na kutofautisha ilani na wagombea wa vyama tofauti; na
Sita, na muhimu kuliko yote, ni mfumo wa Uchaguzi ulio Rafiki kwa wadau wote, kwa maana ya uwanja tambarare kwa ajili ya mechi ya kisiasa inayojumuisha ugawaji wa majimbo, uandikishaji wa wapiga kura, uendeshaji wa kampeni, upigaji wa kura na utangazwaji wa matokeo.
Kwa mujibu wa Mnyika, tofauti na kauli ya Rais Samia iliyotolewa juzi wakati wa sikukuu ya Idd, mabadiiko yanayokidhi viwango hivi bado hayajfanyika.
Aidha, mkutano huo ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti Joh Heche, na Viongozi wengine wa kitaifa.
Watia nia walikubaliana na hoja zote na kusaini petisheni ya kuunga mkono mpango wa "no refrom no election," yaani "hakuna uchaguzi kabla ya mabadiliko."