Strawberry
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 274
- 108
Habari wana Jamii Forum.
jamani Jamani hata sijui nianzie wapi jamani.Ila nawashukuruni kwa sala zenu na maombi yenu.
Tumemaliza msiba wa Mme wangu mpendwa salama.Namwombea Mungu ampe pumziko la milele.
Kweli nashukuruni wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine adi kumafanikisha mkumpuzisha salama Marehemu Mme wangu.Japo ni ngumu sana kwa upande wangu kuamini kama kweli nimeondokewa na Mme wangu ila sina budi kumshukuru Mungu baba.Kweli ntalia siku zote za maisha yangu maana nimeachwa bado umri wangu mdogo na bado nilikuwa nategemea yeye aniongoze katika maisha haya.
Lakini sina budi ya kufunga mkanda na kupigana kiume adi nikuze watoto wangu tuliobahatika kupata na Mme wangu.
Nawasihi wanandoa jamani pendaneni na heshimianeni kila mmoja aone umuhimu wa mwenzie.Hata kama ni chongo hana mvuto jamani siku akikutoka ni majuto tu jamani.
Asanteni sana
jamani Jamani hata sijui nianzie wapi jamani.Ila nawashukuruni kwa sala zenu na maombi yenu.
Tumemaliza msiba wa Mme wangu mpendwa salama.Namwombea Mungu ampe pumziko la milele.
Kweli nashukuruni wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine adi kumafanikisha mkumpuzisha salama Marehemu Mme wangu.Japo ni ngumu sana kwa upande wangu kuamini kama kweli nimeondokewa na Mme wangu ila sina budi kumshukuru Mungu baba.Kweli ntalia siku zote za maisha yangu maana nimeachwa bado umri wangu mdogo na bado nilikuwa nategemea yeye aniongoze katika maisha haya.
Lakini sina budi ya kufunga mkanda na kupigana kiume adi nikuze watoto wangu tuliobahatika kupata na Mme wangu.
Nawasihi wanandoa jamani pendaneni na heshimianeni kila mmoja aone umuhimu wa mwenzie.Hata kama ni chongo hana mvuto jamani siku akikutoka ni majuto tu jamani.
Asanteni sana