Approaches za Mkuu: Tatizo limeanzia hapa

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,071
Kwa sehemu kubwa wananchi wamekuwa wakilalamikia approaches za Mkuu hasa ktk mambo yanayohusu siasa na utawala!
Haya ndio maeneo yanayomdhoofisha boss kisiasa!
  1. Kuhisi kuwa wapinzani ni maadui!
    • Hivi juzi alipokuwa anawaapisha baadhi ya viongozi waandamizi ktk maeneo ya wananchi alisema baadhi ya maneno ambayo sikuweza kuyanukuu kwa ufasaha Ila kiujumla yalisound hivi-"Nimekuwa nikisoma katika baadhi ya mitandao ya kijamii na kugundua kwamba maadui zetu wanalalamika! Sasa ukiona adui yako anakusifia lazima ujitazame wapi unapokosea!" Sina uhakika wa nukuu ya word to word Ila concept nzima ndio ilikuwa hivyo!
    • Katika mazingira ya kuona wapinzani ni maadui, sidhani kama tutajenga tena taifa! Hapa panakupa picha ya yanayotokea jumba tukufu yameratibiwa wapi! Utagundua kuwa ambao hamkualikwa jumba jeupe mnachukuliwaje! Na ile falsafa ya mnajenga nyumba moja kwanini mgombee fito ilishaondoka na yule "mswahili"! This time hatuna dialogues za chochote, tupo ktk robbot mode, just do as ulivyosetiwa na program!
  2. Kukosa uvumilivu anapokerwa na jambo.
    • Hili tumeliona toka alipokuwa na wadhifa mdogo, Mara kadhaa amekuwa akimlaumu mkubwa wake kwa kupenda kusikiliza na kuchelewesha mambo! Yeye ana hardcore approaches na angependa vitu viwe hivyo! Ni rahisi kuwa na hulka hizo unapo ongozwa na mtu Ila wewe ukiwa kiongozi it doesn't work that way! Utaumiza watu wengi!
    • Mkuu kila anayemkosea hana simile, atadeal na wewe on the spot regardless ya madhara yatakayokukuta baada ya maamuzi yake! Wote tunakumbuka wakati wa ubatizo wa daraja, Yule aliyetoa takwimu tata za hewa, wale waliokosa sifa za shule kubwa na hata aliyekunywa mvinyo ktk jengo tukufu la nchi! Mambo ya namna hii huwa yana demoralise watu, hata wale waliobaki frontline bado wana wasiwasi kwa hiyo wanaishi kwa mitego! Hawawezi kuwa wabunifu, ukiwapa report wanaogopa kuiforward maana hawana uhakika na usahihi wake, lkn pia hata kwenye kutoa matamko na miongozo wanaogopa wasije kinzana na boss wao!
Si vibaya kuwa na misimamo yako, lkn ktk siasa bado unapaswa ubalance mipango yako na ile ya taifa! Whatever we are doing ni kwa National interest na sio ili tuje kukumbukwa kwa tuliyoyatenda! Ule msingi Mkuu ukiwa sawa definitely utakumbukwa lkn primary target haiwezi kuwa personal goals!
Wengi tunaolia humu ni sehemu ya mafanikio yako, kila mtu hata wewe mwenyewe you had only one vote ambayo isingekupeleka popote! Tulidhani utafikia malengo pamoja nasi, lkn sasa unajitahidi kutaka kuyafikia malengo peke yako! Wengine wanadhani kuna watu hawapaswi kuaminiwa kwa sasa labda wanaweza kuwa hawampendi Mkuu, lkn tukutane miaka 4 ijayo, mtatutaka tujenge wotee, mtajiona hamtoshi Ila sasa mnajisahau!
Ok! Boss hata wapinzani wanakutakia mema tu, huko wapo kwa tofauti za kiitikadi na uelewa au matarajio mbalimbali, you need them leo ili wakusaidie ktk kujenga, na utawahitaji baadhi yao ili kura zitoshe ni kama pale ulipokuwa akiwaomba kula ulikuwa unasema wewe ni wa wote, maana lengo ni moja kujenga nchi imara!
Just angalia clips zako za campaign na uje uwaombe radhi baadhi ya watu waliokuwa upinzani yet walikupigia bila ya kukuona adui!
Ni maoni yangu tu, unaweza kuwa na maoni yako it is OK! Kwangu ccm na ukawa vyote ni vyombo tu vya kusafiria lkn lengo kuu ni kufikia safari yetu kwa wakati na usalama!
 
Back
Top Bottom