Apple yaamrishwa kuifungua simu ya muuaji

Primier

Member
Joined
Dec 16, 2015
Posts
86
Reaction score
14

Image caption Muuaji wa San Bernadinho Syed Farook
Jaji mmoja katika jimbo la Carlifonia nchini Marekani ameiamrisha kampuni kubwa ya Teknolojia ya Apple kusaidia polisi katika kuchunguza simu ya mwanamume ambaye aliwapiga risasi watu 14 katika eneo la San Bernardino mwezi Disemba.


Syed Rizwan Farook na mkewe waliuawa na polisi baada ya kisa hicho.

Jaji alisema kuwa kampuni ya Apple ni lazima itoe msaada wa kiteknolojia baada kushindwa kuweka nywila ya simu hiyo kwa mara kumi. . Kampuni hiyo bado haijatoa tamka lolote na ina muda wa siku tano kupinga uamuzi huo.


Tangu kutolewa kwa programu mnamo mwezi Septemba 2014,data ya simu za Apple kama vile ujumbe na picha zimewekewa usalama wa kutosha.

Hii ina maanisha kwamba iwapo simu hiyo imefungwa ,ni nywila au neno la siri la simu hiyo linaloweza kuifungua na kupata data hiyo.

Image copyright Reuters
Image caption Simu ya Apple
Iwapo mtu atajaribu mara 10 bila mafanikio data iliopo ndani ya simu hiyo hujifuta .

Hakuna mtu ama hata kampuni ya Apple itaweza kupata ujumbe huo,hatua ambayo kampuni hiyo ilifanya kufuatia ufichuzi wa bwana Edward Snowden kwamba serikali ya Marekani imekuwa ikidukua simu za raia.
 


(news update)Apple yapinga amri ya kuifungua simu ya muuaji


Image copyright Getty
Image caption Mkurugenzi mkuu wa Apple Tim Cook
Apple itapinga amri ya mahakama ya kuwasaidia wachunguzi wa shirika la kijasusi nchini Marekani FBI kuchukua habari katika simu ya muuaji wa watu 14 katika eneo la San Bernadinho nchini Marekani.


Kampuni hiyo ilikuwa imeamrishwa kulisaidia shirika hilo la FBI kuifungua simu ya aina ya iphone ya Farook Syed ambayo wanasema ina habari muhimu.

Katika taarifa ,mkurugenzi mkuu wa Apple Tim Cook amesema:Serikali ya Marekani inaitaka Apple Kuchukua hatua kama hizo ambazo zinatishia usalama wa wateja wetu.


Image copyright AP
Image caption Farook na mkewe
Tunapinga amri hiyo ambayo ina athari zaidi ya kesi iliopo.

Tangu kutolewa kwa programu mnamo mwezi Septemba 2014,data ya simu za Apple kama vile ujumbe na picha zimewekewa usalama wa kutosha.

Hii ina maanisha kwamba iwapo simu hiyo imefungwa ,ni nywila au neno la siri la simu hiyo linaloweza kuifungua na kupata data hiyo.

Image copyright Reuters
Image caption Kampuni ya Apple
Iwapo mtu atajaribu mara 10 bila mafanikio data iliopo ndani ya simu hiyo hujifuta .

Hakuna mtu ama hata kampuni ya Apple itaweza kupata ujumbe huo,hatua ambayo kampuni hiyo ilifanya kufuatia ufichuzi wa bwana Edward Snowden kwamba serikali ya Marekani imekuwa ikidukua simu za raia.
 
Yaani Apple wata i turn hii ishu kua marketing agenda kwamba product zao are more secure and no one can hack them na privacy is 100% hata FBI cant access your details!! big up Apple geniuses
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…