Heart Wood.
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 982
- 1,179
Maisha halisi na pekee kwa Mwanadamu ni yale ya kuwa Mcha Mungu, yaani kutii maagizo ya Mungu. Mambo mengine tuyaonayo hapa Duniani ni ubunifu tu wa Mwanadamu wa namna ya kuishi katika hii Dunia,ambayo kwa kiasi kikubwa hupelekea kumuasi Mungu.
Mabadiliko au Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia ni njia rahisi zaidi ya kuingamiza Nafsi ya Mwanadamu ili isifikie ile hatma ya kweli iliyo kusudiwa.
Mafanikio au thamani ya maisha haipo katika misingi ya kufanikiwa kielimu, kufanikiwa kuwa na uelewa mkubwa wa Falsafa au Saikolojia kuhusu maisha ya Mwanadamu katika misingi ya ubinadamu au kufanikiwa kwa kuwa na kazi nzuri wala kufanikiwa kwa kuwa na utajiri mkubwa au kuwa mtu maarufu zaidi Ulimwenguni.
Iwapo thamani ya maisha ingetafsiriwa katika misingi ya mafanikio kupitia sababu tajwa hapo juu, basi walio jaliwa kuwa namna hiyo, wangeweza pia kutueleza kesho yetu itakuwa ya namna gani, au wangeweza hata kujiongezea siku za maisha yao au kuepuka kifo haswa kile kinachotokea kabla ya mtu kufikia hali ya uzee.
Mafanikio au thamani pekee ya mwanadamu yapo katika misingi ya kumjua Mungu, kufahamu maagizo yake, kuyashika na kuyatenda.
Si kila mwanadamu amejaaliwa kufahamu haya, ila Neema hii ni kwa walio wachache. Mwenye Masikio na Asikie.
Mabadiliko au Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia ni njia rahisi zaidi ya kuingamiza Nafsi ya Mwanadamu ili isifikie ile hatma ya kweli iliyo kusudiwa.
Mafanikio au thamani ya maisha haipo katika misingi ya kufanikiwa kielimu, kufanikiwa kuwa na uelewa mkubwa wa Falsafa au Saikolojia kuhusu maisha ya Mwanadamu katika misingi ya ubinadamu au kufanikiwa kwa kuwa na kazi nzuri wala kufanikiwa kwa kuwa na utajiri mkubwa au kuwa mtu maarufu zaidi Ulimwenguni.
Iwapo thamani ya maisha ingetafsiriwa katika misingi ya mafanikio kupitia sababu tajwa hapo juu, basi walio jaliwa kuwa namna hiyo, wangeweza pia kutueleza kesho yetu itakuwa ya namna gani, au wangeweza hata kujiongezea siku za maisha yao au kuepuka kifo haswa kile kinachotokea kabla ya mtu kufikia hali ya uzee.
Mafanikio au thamani pekee ya mwanadamu yapo katika misingi ya kumjua Mungu, kufahamu maagizo yake, kuyashika na kuyatenda.
Si kila mwanadamu amejaaliwa kufahamu haya, ila Neema hii ni kwa walio wachache. Mwenye Masikio na Asikie.