Mama Kilango si mtu wa maana sana linapokuja swala la uongozi bora, lakini kwa hakika Serukamba ana matatizo makubwa. Hadi sasa sijaelewa wenyeviti wa hizi kamati za bunge wanapatikana kwa kutumia vigezo gani? Serukamba ndiye alikuwa mpiga debe mkubwa kwa TPA ili wale watoa rushwa wa kimataifa CCCC wapewe kazi ya kujenga gati kwa 'usanii' wa mkopo nafuu toka EXIM BANK- China.
Pia Serukamba kama mwenyekiti wa kamati ya miundo mbinu ambayo inahusika pia na sekta ya mawasiliano sijamsikia akisema chochote kuhusu Vodacom ukwepaji wa kodi. Na hapa ndipo madai ya Mama Kilango yanaweza kutupa hisia kuwa Serukamba anasimamia maslahi ya watu fulani fulani.
Lakini kubwa kwangu ninaloona ni kuyumba kwa maadili kwa hizi kamati za bunge. Mbunge wa Bahi (CCM) ana kesi mahakamani, yuko mwenyekiti mwingine amepelekwa Japan na TBS ili awasafishe wakubwa wa TBS! Na week hii tunaambiwa ndugu Chenge kapata uenyekiti wa kamati ya fedha! Chenge alilazimika kujiuzulu kwa sababu wakubwa wake na wananchi pia walikosa 'confidence' kwamba ni mtu safi. Sasa waliomchagua wanapingana na wananchi?
Kwa kifupi, CCM wameonesha ujasiri wa hali ya juu wa kuziba masikio na kufumba macho. Wanakwenda kinyume na matakwa ya wananchi ambao ndio wenye mamlaka ya mwisho nchi hii. CCM wamepata wapi hiki kiburi?