Wa Mjengoni
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 480
- 128
Viongozi wa dini na walokole wenzangu Bwana Yesu Asifiwe!
Naomba kabla hatujaombea Katiba iliyopendekezwa ipite kujaribu kwanza kuangalia vipengele vilivyoko humo kama vina reflect kumtumikia shetani au laa. Mfano jana Jaji Warioba amesema upande wa tunu na maadili ya viongozi Katiba pendekezwa haiwazuii kujirundikia mapesa haramu nje ya nchi, yaani ruksa.
Sasa Mlokole unapoombea kwa dhati kabisa mpaka unalia jambo hili una maana gani kama sio sawa na kumuombea jambazi anayetaka kwenda kuvunja duka afanikiwe? Najua wengi wanaomba bila kufahamu sawasawa wanayoyaombea ndani ya hiyo pendekezwa.
Nimesema hili kwa sababu leo asubuhi nimeona Ch. 10 taarifa ya habari maombezi ya Kanisa la Moraviani Katavi.
Ni bora maombi yakaishia katika kusema "Mungu tuongoze ktk kupata Katiba bora" finish...bila kuongeza neno "iliyopendekezwa."
Mungu awabariki na awape hekima.
Naomba kabla hatujaombea Katiba iliyopendekezwa ipite kujaribu kwanza kuangalia vipengele vilivyoko humo kama vina reflect kumtumikia shetani au laa. Mfano jana Jaji Warioba amesema upande wa tunu na maadili ya viongozi Katiba pendekezwa haiwazuii kujirundikia mapesa haramu nje ya nchi, yaani ruksa.
Sasa Mlokole unapoombea kwa dhati kabisa mpaka unalia jambo hili una maana gani kama sio sawa na kumuombea jambazi anayetaka kwenda kuvunja duka afanikiwe? Najua wengi wanaomba bila kufahamu sawasawa wanayoyaombea ndani ya hiyo pendekezwa.
Nimesema hili kwa sababu leo asubuhi nimeona Ch. 10 taarifa ya habari maombezi ya Kanisa la Moraviani Katavi.
Ni bora maombi yakaishia katika kusema "Mungu tuongoze ktk kupata Katiba bora" finish...bila kuongeza neno "iliyopendekezwa."
Mungu awabariki na awape hekima.