mr pipa
JF-Expert Member
- Jul 26, 2021
- 2,330
- 4,853
Nimestushwa na kauli ya hiyi ya huyu jamaa yangu, kaniambia toka amemuoa, leo wana miaka mitano lakini hali yao kiuchumi ipo vile vile zaidi ya kuongeza vikombe, sufuria na mandoo, na kikubwa anacholalamika jamaa kila mshahara ukipanda, mke naye anaongeza ndugu zake, waje wakae ndani ya nyumba yake mpaka inafikia jamaa anakosa hata uhuru wa kukaa nyumbani kwake mwenyewe amekuwa kama ni mmoja kati ya wanafamilia na sio mume tena, maana kuna muda vikao vya familia ya mke hufanyika kwake na wala hapewi taarifa yoyote, basi baada ya kuniambia haya nikamuuliza wazo lako ni nini, akajibu broo kwa nilipofikia bora niongeze mkemwingine hata nikampangie ilimladi niwe na sehemu ya kupumzika, nikamuuliza vipi umejipangaje kiuchumi? akanijibu kwa kamshahara haka haka katagawika hivyo hivyo kuliko nikose amani nisije nikafa mapema nikamuuliza kwanini usimpe talaka huyu wa kwanza akanijibu kimila yetu kuacha ni ngumu, narud kwenu wakuu hivi inawezekana mwanamke akawa sababu ya kutopanda kiuchumi, je unamshaul vp jamaa