Anahitajika Mwalimu wa Usindikaji Vyakula (Food Processing/Technology)

Boreless

Member
Aug 25, 2009
61
39
Anahitajika mtu mwenye ujuzi wa forumala/recipes zinazotumika kusindika vyakula na viungo mbalimbali kama Garlic Paste, Gindger Paste, Tomato Paste, Mango Pickles, Mayonnaise, Tea Masalla, Pilau Masalla, n.k. Sifa kuu ni ujuzi na si vyeti wala muda wa muombaji kukaa dalasani. Muombaji awe amewahi au anazalisha bidhaa zinazounzwa madukani.

Mwenye ujuzi awasiliane na upegra at gmail.com
 
Sasa kama sifa kuu sio vyeti,huyo mnateka nyie alisomeshwa na malaikla au?
Yaani wewe ndio Kampuni imekuteuwa kabisaa uweke Tangazo kihuni namna hii,hii inaonyesha ni jinsi gani watu mnavyoenda kikanjanja kwenye biashara.
Na biashara kama hizi wakenya ndio maana wanatukimbiza.

Mtu yoyote anapohitajika kwenye ajira kwanza anaulizwa vyeti ili kujua elim yake then experience ndio inafuata.
Sasa ukisema sifa sio vyeti ila ujuzi,we unategemea nini,sio ndio wale mnaoleta Madaktari vimeo muhimbili na hospitali nyingine kufanya vituko kila siku?Na wakiulizwa wanakiri kwamba wao ni wazoefu

Na kama mnaajiri kwa style hiyo mtafunga biashara muda sio mrefu,au watakuja kwenzenu wachukue seko lenu kisha mbakie na fitna na majungu tu.

Teknolojia ya usindikaji inabadila kila naada ya muda,sasa alieenda darasani vizuri na akautumia muda vizuri haya yote anayajua,na ndio maana kuna tofauti ya aliesoma usinidkaji miaka ya 90 na aliesoma kwa miaka kuanzia 2005.
 
Zanzibar Spices LIFE IS HOW YOU THINK AND MAKE IT

Hakuna shuruti kwa yeyote kupoteza muda na na kujaza server ya JF kwa mchango usio na tija. Umewahi kumuuliza Yaya wako au mkeo cheti kwa mapishi anayokuandalia? Wafanyakazi alioanza nao Bakheresa walikuwa na Degree ngapi? Mie nikuombe tu ukiona thread yangu, mchango wako baki nao. Sijawahi pata mrejesho au mchango chanya toka kwako miaka yote ya kuwa hapa JF kwenye majukwaa ya ujasiriamali na biashara
 
Zanzibar Spices LIFE IS HOW YOU THINK AND MAKE IT

Hakuna shuruti kwa yeyote kupoteza muda na na kujaza server ya JF kwa mchango usio na tija. Umewahi kumuuliza Yaya wako au mkeo cheti kwa mapishi anayokuandalia? Wafanyakazi alioanza nao Bakheresa walikuwa na Degree ngapi? Mie nikuombe tu ukiona thread yangu, mchango wako baki nao. Sijawahi pata mrejesho au mchango chanya toka kwako miaka yote ya kuwa hapa JF kwenye majukwaa ya ujasiriamali na biashara

Huwezi kuona mchango wangu wowote kwa kuwa mie naamini Elim kwanza na ndio maana nipo Kidigital sana na wana analojia kama nyie hatuwezi kwenda sawa.

We leo unafananisha Yaya na Mke kwa mapishi na kulinganisha na Taaluma ya usindikaji kwa Level ya Kibiashara?
Aisee we kiboko,unialike siku ya kufunga kiwanda.Endelea kujiadanganya kwamba Bakhresa hakuwa na Senior Staffs wenye Degree level,pole sana mkuu

Ushauri:
Nenda SUA pale wapo kibaoo,au utapewa address ya wale waliosoma pale ambao wanaendesha biashara zao wenyewe,ila umesema vyeti kwako sio issue hapo mtajuana
Au nenda Veta Chang`ombe pale utapewa list ya wajasiriamali wenye uwezo huo ambao walipitia chuo chao.

Halafu ukienda kupata kibali TFDA na TBS uje utuambie kimechotokea huko,maana unachokimbia ndio huko utakumbana nacho.Shule kwanza Vibali baadae
 
Zanzibar Spices LIFE IS HOW YOU THINK AND MAKE IT

Hakuna shuruti kwa yeyote kupoteza muda na na kujaza server ya JF kwa mchango usio na tija. Umewahi kumuuliza Yaya wako au mkeo cheti kwa mapishi anayokuandalia? Wafanyakazi alioanza nao Bakheresa walikuwa na Degree ngapi? Mie nikuombe tu ukiona thread yangu, mchango wako baki nao. Sijawahi pata mrejesho au mchango chanya toka kwako miaka yote ya kuwa hapa JF kwenye majukwaa ya ujasiriamali na biashara
Anachokuambia mshikaj hapo ni sahihi.huwez kufanya ukanjanja na afya za wananchi...utakwama kwenye usajili tfda pale
 
Anachokuambia mshikaj hapo ni sahihi.huwez kufanya ukanjanja na afya za wananchi...utakwama kwenye usajili tfda pale
Hivi mnajua kusoma kweli? Kuna mahali mie nimesema nazalisha kwa ajili ya kuuza au mnaendeshwa na hisia? Eleweni kujifunza mapishi siyo lazima uanzishe kiwanda. Wanaowapikia majumbani mwenu wamethibitishwa na TFDA au wana vyeti vya TBS? Kwani kila mwenye hobby na mpira ni mchezaji? Msiwe mnadandia mambo. ELEWENI kwanza
 
Hivi mnajua kusoma kweli? Kuna mahali mie nimesema nazalisha kwa ajili ya kuuza au mnaendeshwa na hisia? Eleweni kujifunza mapishi siyo lazima uanzishe kiwanda. Wanaowapikia majumbani mwenu wamethibitishwa na TFDA au wana vyeti vya TBS? Kwani kila mwenye hobby na mpira ni mchezaji? Msiwe mnadandia mambo. ELEWENI kwanza
Ulifanikiwa kupata mtu?
 
Back
Top Bottom