Anachotambia TENDWA ni HIKI...

Maneno tupu hayavunji mfupa. Kuduwaa kwa chura na kukodoa macho hakumzuii ng'ombe kunywa maji. Ndege apigaye biribiri nyingi hawezi kusuka kiota, kumbuka mdomo wake ndio mikono ya kufanyia kazi.

Tendwa ni sawa na upatu uvumao. na asifuye mvua imemnyea. Lakini mwisho Tendwa ni kama la kuvunda lishakosa ubani tena. Au kimsahafu Tendwa ni kama chumvi iliyoharibika, haifai tena ni heri kutupwa barabarani ikanyagwe na wapita njia.

Ukubwa ni dawa lakini kwake ukubwa ni uchuro. Basi ukiona hivo sie watu Tanga twasema keshaliwa huyo.

Ni hadithi iliyokwisha hata ukimghania mwana haimkuni masikio. Laleni salama
 

hahaha! AHSANTE....
 
TenDWA kesha tendwa hana cha kujisumbua maana hata huku uraiani nimejaribu kufanya 'research' majibu ya baadhi ya WATU yanatisha. Wengi wamesema AKIFUTE CHADEMA NDO' ATAJUA AMANI NA VITA BORA NINI.
 
Haya sasa kaumbuka. aliyeua amepandishwa kizimbani, ni Policcm, mbona hawajashika wala kushitaki mwanachama wa Chadema kwa mauwaji? Kwa hiyo Atamke wazi kuwa wanaoua ni Policcm wala siyo Chadema.
 
Tendwa hawezi kufuta mawazo ya watanzania atafuta chama tu na kupiga kura hakujali chama ni box la kupigia kura
 
Hawezi kufuta chama, anafuta USAJILI wa chama.

Sheria inaruhusu judicial review ya uamuzi wake kama anakifutia chama usajili.

Kufanya maandamano ni haki ya Watanzania wote, sio lazima wawe kwenye chama chenye usajili. Ndio maana makundi kama ya waandishi wa habari na ya Waislamu wameweza kuandamana.

CDM is not at the mercy of Tendwa. Kitaweza kuendelea na shughuli zake hata kama Tendwa anakuwa bootlicker wa CCM na kukifutia usajili. And judicial review will follow.

Sheria isiyokuwa ya haki si lazima kuitii. Ingekuwa lazima kutii sheria zote hata zile kandamizi basi, makaburu wangekuwa bado wanatawala.
 
Tumsamehe Tendwa sikuhiyo nadhani alisahau kunywa dozi yake ndo maana akalopoka..Unajua huu ugonjwa ukiacha kunywa dawa tu unakusababishia matatizo.
 

i hope wewe si mwanasheria maana umeichambua kirahisi kama mama muuza
 
Tendwa hawezi kufuta mawazo ya watanzania atafuta chama tu na kupiga kura hakujali chama ni box la kupigia kura

hawezi hata kufuta chama

labda ajaribu kujaribu kufta chama

hivi amepona/
 
Namshauri asiche kunywa dawa zake za BP na Sukari maana akiacha huwa anaropoka sana hadi unaweza ukamshangaa alifikaje hapo??amewatuhumu Chadema kwa kuua...huku Jeshi linampandisha askari wake kwa kosa la kuua makusudi!!haoni aibu??Ukada unamsumbua!!
 
Ni wajibu wake kuvikumbusha vyama vya siasa kufuata sheria na taratibu nyingine, lakini tishio la kutaka kuifuta CHDM au chama kingine chochote ni dalili za kukosa 'confidence' au anatafuta uwanja wa kutaka watu wajue kuwa naye yupo!!!!
 
Mbona Wasira alishatamka hata kabla ya Tendwa kwamba watakifuta chadema. kinachotokea sasa ni mpango mahsusi wa kuiondoa chadema baada ya mbinu nyingine zote za kutengeneza migogoro kushindikana. Tukio la kuuwawa mwangosi lilipangwa ili wasingiziwe chadema na baadaye wafutwe lakini Mungu mkubwa kamera imewaumbua.
 
inaoneakana kweli humu mambumbumbu ni wengi sana, hata baada ya kuwekewa hapo vifungu vinavyompa tendwa mamlaka ya kufuta chama cha siasa bado mnahangaika. Kaz kweli kweli.

ndoto zenu za kuifuta cdm ni sawa na ndoto za alinacha. Macho yamewatoka kama mjs aliyebanwa na mlango. M4c 4rever
 
Kwa usalama na amani ya nchi Tendwa usituletee UCCM hapa! Najua unalinda maslahi ya aliyekuteua ambaye ni rais anatoka SSM, ndiye Boss wako. Na kwa mwenendo huu katiba mpya iweke kabisa kuwa msajili wa Vyama awe independent na ofisi yake pia kwa mantiki hiyo nafasi hiyo itangazwe na si kuteuliwa ili japo la kimataifa lihusike kuchagua anayefaa. Babu zeeka salama usitake kuzeeka kama kamanda Kamuhanda aliyetekeleza matakwa ya boss ili astaafu salama!!! Anaweza kupewa ukuu wa mkoa!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…