Anaandika Mo Dewji kuhusu Jean Ahoua

Anaandika Mo Dewji kuhusu Jean Ahoua

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
19,226
Reaction score
68,242
Wanasimba,

Jean-Charles Ahoua ni mmoja wa wachezaji waliotupa sababu nyingi za kushangilia msimu huu, licha ya vyote amekuwa sehemu ya mafanikio yetu.

Kwa kosa moja lilitokea tunaweza kumsema vibaya leo, ila tukumbuke: hata mastaa wa dunia kama Fernando Torres waliwahi kukosa magoli ya wazi — kwenye mechi kubwa kama Chelsea dhidi ya Manchester United. Hii ni soka. Haya ni mambo ya kawaida kwenye mchezo huu.

Lakini jambo kubwa zaidi ni namna tunavyochagua kusimama baada ya kila tukio. Tunajifunza, tunaimarika, na tunaendelea kupambana.

Mchezo wetu dhidi ya Stellenbosch bado uko mbele. Safari haijaisha. Na huu si wakati wa kulaumiana — ni wakati wa kuungana na kua kitu Kimora.

Simba inajengwa juu ya mshikamano. Tunasimama na Jean-Charles. Tunasimama na kila mchezaji anayejitoa kwa jezi hii. Na tunaendelea na vita iliyokua mbele yetu. #HatushiiHapa 📌

Simba ni familia. Simba ni nguvu moja.

#NguvuMoja #SimbaSC #JeanCharles
 
Well said. Lakini Ahoua hawezi kutufikisha kwenye nchi ya ahadi. Wapambane Feisal aje Simba
Feisal hawezi kwenda timu yoyote zaidi ya Simba kwa hapa labda atoke nje ya nchi...hata huko utopolo walipomtukania mama yake mzazi hawezi maisha kurudi kucheza..na njia pekee ya yeye kwenda timu nzuri barani afrika nje ya Tanzania ni kucheza Simba sports club.
 
Well said. Lakini Ahoua hawezi kutufikisha kwenye nchi ya ahadi. Wapambane Feisal aje Simba
Unajua ni kweli jamaa kakosea ila ukiangalia na ligi za wenzetu huko yanayofanyika kiwanjani sometimes tunaweza kujiona hatuna subira.

Nimejaribu kuangalia mechi tatu mfululizo za Al Nassr kule Saudia. Kuna yule dogo anaitwa Duran aise anakosa sana magoli ya wazi.

Ukirudi kwenye mechi ya juzi kati ya Inter na Bayern napo utaona first half ilikuwa na makosa mengi kama haya kwenye eneo la ushambuliaji pande zote mbili.
 
Kwanza hao wanaomkomalia Jean Charles Ahoua wamejiuliza hilo goli 1 Simba ililopata limefungwa na nani? Wanashindwa kuyalaumu Machezaji mengine yaliyotokea Uwanjani bila kufunga hata goli 1 wanakuja kumlaumu aliyefunga hilo goli 1 pekee?
 
Timu imeshinda pia imecheza bado watu wanalaumu wachezaji? Kuna watu ni wajinga sana juzi Harry Kane amekosa goli la wazi ambako lingewapeleka Bayern dk 30 za nyongeza na husikii makelele
 
Back
Top Bottom