Shujaa Mwendazake
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 3,734
- 6,292
Arusha. Mkuu wa idara elimu msingi halmashauri ya Jiji la Arusha, Omary Kwesiga amesema ameshangazwa kusimamishwa kazi akidaiwa kufanya igizo la kuchomwa chanjo ya ugonjwa wa Covid-19 .
Amesema picha za video zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa hakuchomwa chanjo hiyo zimechezewa, na kubainisha kuwa alichanjwa.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Ijumaa Agosti 6, 2021 Kwesiga amesema anashangazwa na video hiyo, "nimezuiwa kuongea na vyombo vya habari kulingana na maadili ya kazi na kikubwa mimi nimechanjwa nina ushahidi na nipo Salama."
Ofisa huyo na ofisa muuguzi msaidizi wa hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Scolastica Kanje leo wamesimamishwa kazi na mamlaka zao kwa tuhuma za kufanya igizo la kuchanja.
Kwa takribani siku tatu video hiyo inayomuonyesha Kwesiga na Kanje wakifanya kile ambacho kimetafsiriwa ni maigizo imebua mjadala mitandaoni.
Mwananchi
My Take:
Inaonekana hata waliohukumu walifuata Mhemko tu, Hawakufuata "Natural Justice Principle". Ummy Mwalimu amekimbilia kwenye Media kuclear the air lakini walipaswa kuwahoji.
Muhusika anasema halikuwa Igizo, Waziri anasema lilikuwa Igizo.
Ha ha ha haaa
Amesema picha za video zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa hakuchomwa chanjo hiyo zimechezewa, na kubainisha kuwa alichanjwa.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Ijumaa Agosti 6, 2021 Kwesiga amesema anashangazwa na video hiyo, "nimezuiwa kuongea na vyombo vya habari kulingana na maadili ya kazi na kikubwa mimi nimechanjwa nina ushahidi na nipo Salama."
Ofisa huyo na ofisa muuguzi msaidizi wa hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Scolastica Kanje leo wamesimamishwa kazi na mamlaka zao kwa tuhuma za kufanya igizo la kuchanja.
Kwa takribani siku tatu video hiyo inayomuonyesha Kwesiga na Kanje wakifanya kile ambacho kimetafsiriwa ni maigizo imebua mjadala mitandaoni.
Mwananchi
My Take:
Inaonekana hata waliohukumu walifuata Mhemko tu, Hawakufuata "Natural Justice Principle". Ummy Mwalimu amekimbilia kwenye Media kuclear the air lakini walipaswa kuwahoji.
Muhusika anasema halikuwa Igizo, Waziri anasema lilikuwa Igizo.
Ha ha ha haaa