Nigga What
Senior Member
- May 1, 2021
- 164
- 438
Mimi ni kijana wa miaka 30 naishi Makongo nataka ushauri kidogo. Nilikuwa na mwanamke tulikutana mwaka 2011 nikianza mwaka wa kwanza UDOM lakini mwenzi wangu alisoma Engineering chuo kimoja maarufu Turkey. Tulipendana sana na yule dada kipindi hicho tunawasiliana kwa video calls skype na viber, whatsapp kwa mara ya kwanza nilitumia miaka hiyo na yeye ndiye aliyenifundisha kupitia simu yangu Smart phone ya kwanza Nokia symbian
Tuliendelea namapenzi yetu akawa akirudi likizo anakuja dom tunafanya mambo yetu maisha yanaendelea, tulipanga mipango yetu vizuri ya maisha ya mbele na watotot wetu majina tutajayowapa nk
Baada ya mimi kumaliza chuo 2014 niliingia mtaani nikiwa sina dira naishi nyumbani na nilikua nahaha kutafuta nafasi za kujitolea, na yeye pia alipomaliza alirudi tanzania ila kwa kuwa mzee wake ni kiongozi mwenye network kubwa basi akamuunganisha na kampuni moja maarufu ya engineering hapa bongo.
VITIMBWI VINAANZA: Kuna siku nimeamka zangu asubuhi maeneo ya kimara nilikokuwa nikiishi ilikuwa ni weekend na kitu cha kwanza ilikuwa kumpigia mwenzangu lakini nilishangazwa na maneno aliyoyatoa kuwa kuna mtu amemshauri kuwa mimi siwezi kumuoa kwa sababu jamaa ni mtu wa saikolojia kwa jinsi alivyosimuliwa kuhusu mimi anaona nataka kumchezea huyo binti GADEMITI. Nikamuuliza huyo mtu ni nani akaniambia ni mmoja wa waajiriwa kwenye ofisi yao nikamuuliza mwanamke umewezaji kumwamini huyo mtu wakati mimi na wewe tunajuana vizuri way back, akanijibu kwamba mimi nimebadilila si kama zamani tulivyokuwa aisee nilitamani kulia. Kuanzia hapo kila nikimpigia simu yuko busy na baadae hanitafuti
Nilichanganyikiwa na ufukara jumlisha kufanyiwa kitu kama hicho ni kibaya zaidi kuona post instagram za mwanamke akichumbiwa na mtu yule yule aliyemlisha pete, kuna siku nilitembea kutoka riverside mpaka stop over kimara sikujua hata nimefikaje, niliandamwa na mawazo nikakonda sana
Mungu si athumani nikapata kijisehemu cha kujitolea Mikocheni nilifanya kwa mwaka 1 na miezi 3 nikaajiriwa na kulipwa mshahara wa maana safari kibao per diem zikafurika nalala hoteli nzuri kifupi maisha yakanyooka, mwenzangu akaolewa mapicha kibao marafiki zangu walilaani sana kitendo cha mwanamke yule.
Mwaka 2019 nilikua kibonge hatari maana nilikua nakula na kunywa bia sina stress mrembo akikatiza mbele napita nae na ofisini kwa mwezi naingia siku 12 tu the rest ni kula maisha nikakopa na kagari ka mjapan kapremio kwahiyo full kipupwe
KARMA KAANZA MAMBO YAKE: Nikiwa maeneo ya MIKOCHENI tanesco nilikutana na yule mwanamke akiwa na mwenzi wake alishituka sana mpaka mwenzi wake alihisi kitu mimi aikujali nikawasha ndinga nikateleza lakini baadae niliona dm instagram akinishangaa kunenepa nilipoangalia instayake nilikuta amefuta zile picha za engagement na ndoa zote, aliniomba namba yangu DM na akanipigia akiwa mnyonge sana
Niliamua kumkwepa kwa muda kwa sababu huwa nina huruma sana na huruma yangu inaweza kuleta maafa baadae, wiki aliyopita ameniandikia sms kuwa mtu wake amebadilika sana na anaomba ushauri anakuja MAKONGO makazi yangu mapya nimshauri.
Nifanyaje ndugu zangu?
Hii ni stori ya mfanya kazi mwenzangu ilionisisimua sana, ushauri wako ni muhimu tafadhali.
Tuliendelea namapenzi yetu akawa akirudi likizo anakuja dom tunafanya mambo yetu maisha yanaendelea, tulipanga mipango yetu vizuri ya maisha ya mbele na watotot wetu majina tutajayowapa nk
Baada ya mimi kumaliza chuo 2014 niliingia mtaani nikiwa sina dira naishi nyumbani na nilikua nahaha kutafuta nafasi za kujitolea, na yeye pia alipomaliza alirudi tanzania ila kwa kuwa mzee wake ni kiongozi mwenye network kubwa basi akamuunganisha na kampuni moja maarufu ya engineering hapa bongo.
VITIMBWI VINAANZA: Kuna siku nimeamka zangu asubuhi maeneo ya kimara nilikokuwa nikiishi ilikuwa ni weekend na kitu cha kwanza ilikuwa kumpigia mwenzangu lakini nilishangazwa na maneno aliyoyatoa kuwa kuna mtu amemshauri kuwa mimi siwezi kumuoa kwa sababu jamaa ni mtu wa saikolojia kwa jinsi alivyosimuliwa kuhusu mimi anaona nataka kumchezea huyo binti GADEMITI. Nikamuuliza huyo mtu ni nani akaniambia ni mmoja wa waajiriwa kwenye ofisi yao nikamuuliza mwanamke umewezaji kumwamini huyo mtu wakati mimi na wewe tunajuana vizuri way back, akanijibu kwamba mimi nimebadilila si kama zamani tulivyokuwa aisee nilitamani kulia. Kuanzia hapo kila nikimpigia simu yuko busy na baadae hanitafuti
Nilichanganyikiwa na ufukara jumlisha kufanyiwa kitu kama hicho ni kibaya zaidi kuona post instagram za mwanamke akichumbiwa na mtu yule yule aliyemlisha pete, kuna siku nilitembea kutoka riverside mpaka stop over kimara sikujua hata nimefikaje, niliandamwa na mawazo nikakonda sana
Mungu si athumani nikapata kijisehemu cha kujitolea Mikocheni nilifanya kwa mwaka 1 na miezi 3 nikaajiriwa na kulipwa mshahara wa maana safari kibao per diem zikafurika nalala hoteli nzuri kifupi maisha yakanyooka, mwenzangu akaolewa mapicha kibao marafiki zangu walilaani sana kitendo cha mwanamke yule.
Mwaka 2019 nilikua kibonge hatari maana nilikua nakula na kunywa bia sina stress mrembo akikatiza mbele napita nae na ofisini kwa mwezi naingia siku 12 tu the rest ni kula maisha nikakopa na kagari ka mjapan kapremio kwahiyo full kipupwe
KARMA KAANZA MAMBO YAKE: Nikiwa maeneo ya MIKOCHENI tanesco nilikutana na yule mwanamke akiwa na mwenzi wake alishituka sana mpaka mwenzi wake alihisi kitu mimi aikujali nikawasha ndinga nikateleza lakini baadae niliona dm instagram akinishangaa kunenepa nilipoangalia instayake nilikuta amefuta zile picha za engagement na ndoa zote, aliniomba namba yangu DM na akanipigia akiwa mnyonge sana
Niliamua kumkwepa kwa muda kwa sababu huwa nina huruma sana na huruma yangu inaweza kuleta maafa baadae, wiki aliyopita ameniandikia sms kuwa mtu wake amebadilika sana na anaomba ushauri anakuja MAKONGO makazi yangu mapya nimshauri.
Nifanyaje ndugu zangu?
Hii ni stori ya mfanya kazi mwenzangu ilionisisimua sana, ushauri wako ni muhimu tafadhali.