HKigwangalla
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 722
- 971
Ajira Kwanza Vs Elimu Kwanza...
Mwaka 1994, Bwana Tony Blair alikuwa kiongozi mkuu wa upinzani Bungeni. Mwaka 1997 alikiwezesha chama chake kushinda nafasi ya uwaziri mkuu, na yeye akawa waziri mkuu. Aliweka kipaumbele cha kwanza, elimu, cha pili, elimu na cha tatu elimu. Mhe. Edward Lowassa jana ameeleza kuwa #AjiraKwanza siyo muhimu, na badala yake #ElimuKwanza ndiyo. Mjadala wa ajenda ndiyo haswa unahitajika kwenye majukwaa ya siasa zetu katika zama hizi. Sikubaliani naye kabisa. Nikiamini mfano anaoiga haukai kwenye ulinganifu sawia, sababu, Uingereza ya mwaka 1997, Mei, Bw. Blair alipoingia madarakani ni tofauti sana na Tanzania ya 2015. Uingereza ya Bwana Blair haikuwa na changamoto ya usalama wa chakula, changamoto ya ajira na wala changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi na ukosefu wa mvua kama Tanzania yetu ya 2015. Pamoja na kuthamini elimu na ukombozi wote unaokuja nayo, bado tu ukweli utabakia kwamba mtu hauwezi kupeleka shule mtoto mwenye njaa! Ama hauwezi kulipa ada ya shule wakati nyumbani hauna uhakika wa chakula.
Msingi wa pendekezo la kipaumbele changu cha #AjiraKwanza ni kwamba, kwa vyovyote vile ni lazima tupambane kuondoa umaskini na kukuza uchumi kwa malengo ya kuzalisha ajira za kutosha. Na ili tufikie malengo yetu kwa haraka, ajira tunazotakiwa kuzalisha zinapaswa zitokane na kilimo, viwanda vidogo vidogo vyenye linkage na kilimo na kuimarisha masoko ya bidhaa za shambani na za viwanda vyenye uhusiano wa moja kwa moja na kilimo. Tukifanya haya tutaajiri watu wengi zaidi, tutajihakikishia uhakika wa chakula, tukikuza biashara ya ndani tutakusanya kodi kwa watu wengi zaidi na uchumi ukiimarika ndipo sasa tutaweza kuboresha huduma za elimu, afya na maji kwa uhakika zaidi, tutakuza uchumi kwa haraka zaidi na uchumi utawagusa watu wengi kwa mara moja, tutapunguza uagizaji wa bidhaa toka nje - zaidi ya yote haya, hili ni wazo linalotekelezeka!
Mwaka 1994, Bwana Tony Blair alikuwa kiongozi mkuu wa upinzani Bungeni. Mwaka 1997 alikiwezesha chama chake kushinda nafasi ya uwaziri mkuu, na yeye akawa waziri mkuu. Aliweka kipaumbele cha kwanza, elimu, cha pili, elimu na cha tatu elimu. Mhe. Edward Lowassa jana ameeleza kuwa #AjiraKwanza siyo muhimu, na badala yake #ElimuKwanza ndiyo. Mjadala wa ajenda ndiyo haswa unahitajika kwenye majukwaa ya siasa zetu katika zama hizi. Sikubaliani naye kabisa. Nikiamini mfano anaoiga haukai kwenye ulinganifu sawia, sababu, Uingereza ya mwaka 1997, Mei, Bw. Blair alipoingia madarakani ni tofauti sana na Tanzania ya 2015. Uingereza ya Bwana Blair haikuwa na changamoto ya usalama wa chakula, changamoto ya ajira na wala changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi na ukosefu wa mvua kama Tanzania yetu ya 2015. Pamoja na kuthamini elimu na ukombozi wote unaokuja nayo, bado tu ukweli utabakia kwamba mtu hauwezi kupeleka shule mtoto mwenye njaa! Ama hauwezi kulipa ada ya shule wakati nyumbani hauna uhakika wa chakula.
Msingi wa pendekezo la kipaumbele changu cha #AjiraKwanza ni kwamba, kwa vyovyote vile ni lazima tupambane kuondoa umaskini na kukuza uchumi kwa malengo ya kuzalisha ajira za kutosha. Na ili tufikie malengo yetu kwa haraka, ajira tunazotakiwa kuzalisha zinapaswa zitokane na kilimo, viwanda vidogo vidogo vyenye linkage na kilimo na kuimarisha masoko ya bidhaa za shambani na za viwanda vyenye uhusiano wa moja kwa moja na kilimo. Tukifanya haya tutaajiri watu wengi zaidi, tutajihakikishia uhakika wa chakula, tukikuza biashara ya ndani tutakusanya kodi kwa watu wengi zaidi na uchumi ukiimarika ndipo sasa tutaweza kuboresha huduma za elimu, afya na maji kwa uhakika zaidi, tutakuza uchumi kwa haraka zaidi na uchumi utawagusa watu wengi kwa mara moja, tutapunguza uagizaji wa bidhaa toka nje - zaidi ya yote haya, hili ni wazo linalotekelezeka!