Ajali mbaya Ndanda masasi

Hii habari imenisikitisha sana baada ya kusikia mmojawapo ya aliyekufa ni afisa kilimo niliyewahi fanya naye kazi fulani hapo Mangaka. Wapate pumziko la milele.........amina.
 
Mita 15 kutokea hospitali?
Ina maana ni pale darajani kama unaelejea masasi au pale getini kama unatokea ndanda madukani?
 
Pole sana Dr Robert aka Higush aka Muzushi my classmate and intern mate. Mungu akupe nguvu upone haraka.
 
Naomba kujua majina ya Majeruhi na Waliofariki.

Kaka Yangu anafanya kazi wilaya ya Nanyumbu.
Vp umesikia chochote mpaka muda huu about ur bro? Umewasilianan nae?
Afueni umekumbuka majina yao....
Unaweza kunitajia majina ya marehemu?
Hapo juu jamaa kawataja baadhi mi siwajui kabisa...Jaribu kufuatilia kwa ukaribu sana.
 
Picha hizo, kwa hisani ya mdau mmoja kule facebook..........

wasamaria wema wakijitahidi kuwanasua waliokuwa wamenaswa katika gari na maiti zilizonaswa.




 


Hatareeeeeeee sana!!
Kwa kweli hii ni hatari sana ... duh! ajali mpaka Land Cruiser inakatika katikati! ... duh! ... jamaa yaelekea alikuwa anakimbia kwa spidi ya ndege
 
Picha hizo, kwa hisani ya mdau mmoja kule facebook..........

wasamaria wema wakijitahidi kuwanasua waliokuwa wamenaswa katika gari na maiti zilizonaswa.
Mkuu Katavi ... asante kwa picha , ila hii ajali si mchezo nimeziangalia hizo picha nikawa naimagine impact iliyotokea yaani mpaka cruiser inagawanyika vipande!
 
Last edited by a moderator:
Poleni wafiwa,

WILAYA AU TRAFA???

Hizi wilaya NYINGINE MBONA HAZIFAHAMIKI KITAIFA ????

Mbon kuna mikoa mingine haipewi wilaya mpya...
Maswalai haya nadhani ungeyaelekeza kwa JK-the Prezidaa wa JMT.
 
Waliofariki ni Dereva! Anaitwa Mussa likungwa pamoja na afisa kilimo na Mifugo wa wailaya(DALDO) almaarufu mzee Mabiho! Afisa mipango hali sio nzuri, amepata madhara kwenye mbavu na kifua! Anaitwa KAZEE! Pamoja DMO! Robert lyimo amepata madhara kwenye miguu! Na hizi ni baadhi ya picha la tukio lenyewe!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Maswalai haya nadhani ungeyaelekeza kwa JK-the Prezidaa wa JMT.

Ni hoja ndani hoja tu Mkuu. Nchi hii sasa imekatwakatwa na kucharangwa kama vibanzi au chipsi kila mwanasiasa anatengeneze Mkoa wake na Wilaya yake kwa maslahi yake.
 
Speed imechangia sana yanonesha.

usitoe majumuisho ya jumla, imekuwa ni kasumba sasa kila ikitokea ajali inayolaumiwa ni mwendo kana kwamba ni mkali, mimi nafikiri tuishirikishe fizikia ili tuwe na majibu ya kitaalam na sahihi.

vifuatavyo vinaweza kuchangia kusababisha ajali:-
1) ubovu wa barabara (mashimo/makorongo kwenye lami)
2) watumiaji wengine wa barabara
3) kutokuwepo kwa vibao vya ishara pembezoni mwa barabara
4) mchanga/vikokoto kwenye barabara za lami.
n.k
 
Mkuu tumejuisha 'speed' kutokana muonekano wa gari baada ya ajali-impact ilikuwa kubwa(Head collision), Kama unayajua maeneo ya Ndanda Pale hamna ubovu wa barabara, na hata vikokoto hamna(Asphalt road),ni straight road njia ya masasi baada ya ile Junction ya kwenda hospital, sio sehemu risk kwa ajali na ni miaka mingi haijawahi kutokea ajali pale.
Labda uniambia ubovu wa gari(Mechanical Factor) au dereva mwenyewe(ambapo naamini alikuwa mzoefu sana wa hiii njia).
 
Kwa jinsi eneo lilivyo nadhani na spidi nayo ilichangia au ubovu wa gari kama ulivyosema.
 
Kaka naomba kama umekumbuka hilo jina itakuwa vyema kama utalitaja hapa.

Nina kaka yangu ni HR anafanya kazi wilaya ya Nanyumba anafahamika kwa Surname ya Ndinda, Je alikuwepo? Naomba kujuzwa tafadhari.



Kwanini usifanye utaratibu wa mawasiliano ya simu ya huyo kaka yako kwa yeye mwenyewe, Mke wake(kama ameoa) na Marafiki zake wa karibu wa huko Nanyumbu. kwanza anza kujua kama naye alikuwa kwenye msafara wa bajeti au alibaki Nanyumbu akisukuma Madokezo

Pole kwa wafiwa, wale Majeruhi Mwenyezi Mungu awajalie waweze kupona na kurejea katika Afya njema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…