Aishi Manula kwanini lakini?

Jamani wakati mwingine tuwe wakweli Manula amefanya kazi kubwa sana hasa kwenye mechi ya Namibia. Ni kweli Manula ana madhaifu ya kutoka bila mpangilio na udhaifu wa kucheza krosi na kona. Lakini kwenye mechi dhidi ya Namibia alifanya hayo makosa mara moja au mbili tu. Na Manula ndiye aliyeinua morali ya timu nzima kwa kufanya "saves" za maana. Huu Usimba na Uyanga usitufanye tuwe vipofu hata kwenye mambo yaliyo wazi. Na hongera sana kwa benchi la ufundi kwa kuanza na Farid badala ya Mhilu hapo ndio chachu ya ushindi ilipoanzia.
 
Huko Nyoni tunaambiwa karudi nyumbani
 

Attachments

  • IMG-20210125-WA0051.jpg
    42.3 KB · Views: 9

Umekili mwenyewe kuwa ni kweli Manula Ana madhaifu ya kutoka golini na kucheza krosi na Kona udhaifu huo ndio tunataka
 
Japo jamaa anachomaga
Ila mngejua ndo kipa mwenye cleenshit nyingi huko CHAN ..
Anazo 8 mkiona hivyo mjue beki yetu ni mbovu mnooo
 
Naona unaongozwa na chuki au kutokujua.
Kuna faida kubwa sana kipa kutoka golini kuwahi mipira ambayo ingeleta hatari langoni na hiyo imekuwa ikimsaidia sana Manula kuiokoa Simba na Stars pia. Kwa taarifa yako mpaka sasa Manula ndiye kipa anayeongoza kwa uokoaji katika michuano ya CHAN, hiyo inathibitisha ubora wake na faida ya maamuzi hayo unayoyapigia kelele. Makocha wanaona kinachoendelea so kama kuna shida watamueleza na kumuelekeza lkn mpaka sasa bado Manula ni mlinda mlango bora Afrika.
 
Wote tunakubaliana Manula ni Tanzania one Hilo halina ubishi nilicho jaribu kukielezea ni mapungufu yake ili yafanyiwe kazi kabla hatujaanza michuano ya clabu bingwa
 
... Simba iliangalie Hili tatizo la Manula kutoka golini kuwahi Mpira bila hesabu za uhakika. Hili nimeliona sana Stars ilipocheza na Namibia.
Katika kikosi cha Tanzania, hadi sasa mchezaji mwenye rating kubwa huko CHAN ni Aishi Manula. Tafuteni hoja nyingine

 
Huko Nyoni tunaambiwa karudi nyumbani
Kwani uzi unahusu Manula au wachezaji wote wa Simba? Naona chuki imetamalaki haswaa! Kama ishu ni Simba, basi watawakera sana, maana yupo mshangiliaji Morrison special kwa ajili ya kukera tu
 
Kwa hili kosa anahitajika afanyiwe programm maalum.
Nakumbuka Ivo mapunda alikuwa na kosa la kupunch mpira kuelekea kwa mshambuliaji, huu udhaifu uliigharimu timu yake mara kadhaa.
Nafikiri haya makosa yanaweza kurekebishika.
 
Kwa hili kosa anahitajika afanyiwe programm maalum.
Nakumbuka Ivo mapunda alikuwa na kosa la kupunch mpira kuelekea kwa mshambuliaji, huu udhaifu uliigharimu timu yake mara kadhaa.
Nafikiri haya makosa yanaweza kurekebishika.
Umefafanua vizuri sana na ndio lengo la huu uzi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…