Airtel mnatuibia airtime bundle

Airtel mnatuibia airtime bundle

Abuhunna

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
409
Reaction score
233
Habar wanaJamiiForums,

Ni mara kadhaa nimebaini kuwa Airtel wananiibia muda wangu niliojiunga kwa vifurush vya internet, mfano jana jioni nilijiunga kwa kifurushi cha 500/- na kupata mb 300, lakini sikutumia kabisa kifurushi hicho, leo nilipo amka nikaangalia salio nikakuta kuna mb 285.

Chaajabu nilipojiunga na internet nilifanikiwa ku-dowload Mozilla Firefox ambayo kwa ufahamu wangu wa IT hiyo software haizidi hata Mb 100.

Baada ya hapo nilifanikiwa kufungua gazeti la Mwananchi, internet imekata napokea SMS bundle imeisha. Hii inakuwaje kama sio wizi, unapo-comment kurudisha jibu hasi zingatia ninae lalamika hapa ninakautaalam wa IT.

Nawasilisha
 
Mimi kwa sasa hadi nimechoka, kila mala nikinunua bundle la wiki, nakupata sms 300,natumia kama sms 5,naambiwa zimekwisha!!! Unawapigia wanakwambia ni kweli zimekwisha!! Ukiangalia salio sms, wala bundle zinaonyesha 0!!nimewatukana wakinitafuta powa, nimenunua umeme yapata wiki 2,sasa pesa wamekata hadi leo sijapata token! !ukiwapigia eti linashughulikiwa!!
 
Airtel wezi sana, sijui kwa nn TCRA hawasomi malalamiko kama hayoo, achana nao kwa net hamia halotel, mm na enjoy sana
 
Airtel wamechoka me kila cku nalalamika me nitahama mda c mrefu..hawaeleweki ukijiunga mara wanakuambia huna salio..so what!!!
 
Mimi kwa sasa hadi nimechoka, kila mala nikinunua bundle la wiki, nakupata sms 300,natumia kama sms 5,naambiwa zimekwisha!!! Unawapigia wanakwambia ni kweli zimekwisha!! Ukiangalia salio sms, wala bundle zinaonyesha 0!!nimewatukana wakinitafuta powa, nimenunua umeme yapata wiki 2,sasa pesa wamekata hadi leo sijapata token! !ukiwapigia eti linashughulikiwa!!

hata mimi nimenunua umeme majuzi sijapata token hadi sasa niliwapigia walinijibu wanashughulikia,vocha za university napata GB dk 5 tu wakati ni dk 150
 
kweli hata mie nimewastukia waache haka kamchezo

Airtel ni shida si kwenye bundle tu za internet hata kwenye vifurushi vyao vya muda wa maongezi. Nafikiria kuwasiliana na TCRA wawafuatilie. Ni njia rahisi. Ukipewa kifurushi cha muda wa maongezi basi wewe note muda kwa kutumia kifaa kingine. Unapokata simu angalia muda wako uliotumia na ule unaoambiwa na wao kwa sms ni vitu viwili tofauti. Wanaonesha umetumia muda mwingi kuliko uhalisia wenyewe. Huo ni wizi mkubwa. Nadhani kasi ya sekunde yao pengine ni mara tatu ya sekunde ya kawaida. Kwanini wasitoe muda au vifurushi vyenye uhalisia kuliko kupumbaza watu huku ukiwaabia kwa kuset mfumo mwingine usioendana na ukweli. Ni sawa na mtu anayekuuzua mafuta kwenye kifaa ambacho kiko labeled lita kadhaa lakini kiuhalisia ukipima mafuta hayo ama utakuta ni nusu yake. TCRA fuatilieni hilo maana nanyi mna simu. Jaribuni kuchunguza vifurushi vyao vya maongezi na internet
 
Juzi nilijiunga na Airtel bando ya siku ya 1 GB kwa shs 1000.

Cha kushangaza baada ya dakika 3-4 tu kwenye google search, natumiwa meseji bundle imetumika asilimia 90!

Dah! Na kweli baada ya dakika nyingine 2-3 za SUPER SLOW internet speed Airtel bando ya 1 GB ikakata kabisa!

Majambakazi wakubwa! Nimeamua bora nirudi Tigo angalau wana 4G ya ukweli.
 
Habar wanajamii
Ni mara kadhaa nimebaini kuwa Airtel mnaniibia muda wangu niliojiunga kwa vifurush vya internet, mfano jana jioni nilijiunga kwa kifurushi cha 500/- na kupata mb 300, lakini sikutumia kabisa kifurushi hicho, leo nilipo amka nikaangalia salio nikakuta kuna mb 285.
Chaajabu nilipojiunga na internet nilifanikiwa ku-dowload Mozilla Firefox ambayo kwa ufam wangu wa IT hiyo software haizid hata mb 100, baada ya hapo nilifanikiwa kufungua gazeti la mwananchi, internet imekata napokea SMS bundle imeisha.
Hii inakuwaje km sio wizi, unapo-comment kurudisha jibu hasi zingatia ninae lalamika hapa ninakautaalam wa IT
Nawasilisha

we ndo unajua leo?,nunua mb 180 halafu download kitu cha mb 100 uone wizi wa airtell ulivyo
 
Nadhani kulalamika hapa haikusaidii..Toa malalamiko yako sehemu husika..Kituo cha huduma kwa wateja kipo au TCRA Ipo pia..
 
Nadhani kulalamika hapa haikusaidii..Toa malalamiko yako sehemu husika..Kituo cha huduma kwa wateja kipo au TCRA Ipo pia..

Kulalamikia hapa kuna faida yake kwani inaamsha nguvu ya wengie ambao pia wanathibisha dhulma hizo, na hao Airtel wanacho kitengo cha huduma kwa wateja, ambapo shughuli zake ni pamoja na kupokea na kufuatilia malalamiko ya wateja ambayo pia yanapitia kwenye vyombo vingine vyovyote.
Hii ni kusema taarifa hizi huwa zinawafikia
Na kupitia hapa wengine ambao hawaja jiunga nao wanazinduka
 
Back
Top Bottom