Aina za ndoa

timetoloveyourself

JF-Expert Member
Mar 24, 2015
206
206
Katika pita pita zangu nimekutana na maneno haya juu ya aina za ndoa nimeamua nishare nanyi wana jamii.
Angalizo kwa ulie katika aina yoyote tajwa,usijitie hatia ktk hali uliyonayo. Kikubwa mtumainie Mungu upate faraja na amani katika maisha kwa maana yeye ndie msemaji wa mwisho na ikiwa ameruhusu jambo hilo litokee kwako maana yake kwake kuna suluhisho la kudumu.

1⃣ Ndoa ya Uhalamia(Kidnaper Marriages.

Hii ndoa ya watu ambao wamechukuana bila utaratibu maalumu. Mchungaji hafahamu,sheikh au wazazi hawafahamu.

Na wala Hakuna Mahari imetolewa ni ndoa ya uharamia ambao wao tu wawili wanahimizana na kukwapuana kinyemela.
Baadaye watu wengine wanakuja kujua tayari watu wanaishi pamoja.

2⃣ Ndoa ya Ujambazi (Hizi ni ndoa za mtu kulazimishwa) robbery Marriage.
Wazazi wanaamua kumlazimisha binti au kijana kuolewa au kuoa mtu ambaye hampendi.
Inaweza kufikia kiwango hata cha kupingwa na kuwekewa vikwazo ili uolewe au uoe huyo ambaye ni Chaguo lao na Siyo wewe. Kwahiyo mtu anajikuta ameingia kwenye ndoa Akiwa amesukumiwa.

3⃣ Fixed Marriage(Ndoa yenye Masharti ya Vifungo)

Hii ni ndoa ambayo watu wanahimizwa na Ndugu au Wazazi kuwa.

_Unatakiwa uolewe na kabila lako.

_Unatakiwa uoe kabila lako.

_Unatakiwa uoe Ukoo fulani.

_Unatakiwa uolewe na Ukoo fulani.

Na Ukienda kinyume nao Watakuinukia Ndugu wote kukupingana na Unachotaka kufanya na badala yake Unalegea na Kuamua Kuoa au Kuolewa kama Wanavyotaka wao.
Na Ukiwakatalia watatamka laana.
Mfano:
_Ukiolewa hutazaa
Au Ukiolewa Mume wako atakuwa Mto.
_Watoto wako watakuwa Bata.

Wako watu waliingia ndoa za namna hii kuogopa Vita ya Ndugu kuwainukia.

4 ⃣ CATERPILLAR MARRIAGE(Ndoa ya Tingatinga)

Hii ni ndoa ya watu ambao baada ya tu ya Kifunga ndoa wataanza kukabiliana na matatizo. Vifo vya watu wao wa karibu,biashara kuanza kudorola,miradi kuanza kuharibika,Kama ni Mifugo itapata magonjwa na kufa,Kama ni Biashara haiendi tena. Milango yao yotee ya mafanikio imeharibika. Hapo ujue Spirit of CATAPILLAR..

Inatokana na Baadhi yao Hawakuwa wamepata muda wa kuvunja roho za Ufilisi.

Ndio maana semina ya vijana na mafundisho kabla ya ndoa Ni ya muhimu sana. Ili isije kuchelewa mmeingia kwenye ndoa hayo yakawapata mkashangaa nini kimetokea.

PREVENTION IS BETTER THAN CURE.


Tumia somo hili Kujikinga kama bado hujaingia kwenye ndoa na Kama umeshaingia Usijute MTAFUTE MFINYANZI WA AJABU MWAMBIE FINYANGA NDOA HII IKAE VIZURI NA YEYE NI MWAMINIFU ATAIFINYANGA.
5

5⃣ Ndoa ya MTUMBA(Second hand Marriage)

Ndoa ya kuoa au kuolewa na Mtu ambaye tayari alishakuwa ameoa au Ameolewa.

Kuvaa Mtumba lazima uamue Kukubaliana na harufu ya Mtumba.

Ukubaliane na Kiatu cha Mtumba vingine vinakuwa vimeangalia upande.

Ukubaliane nyingine zimeshaunguzwa na Pasi.

Hivyo kuingia kwenye ndoa ya Mtumba Uwe tayati kukubaliana na Jinsi ilivyo.

Ndoa hii huwa ni Kama kulalia Kitanda kikuukuu au Cha Zamani.

Ukubaliane na Kutu na Kunguni wake.

Itabidi ukikungute sana sana mpaka kunguni wote wawe wametoka.

Anyway Hii nayo ni Ndoa na watu wengi wameingia na Kama hawakupata mwongozo bora wataishia Kushangaana na Kuangaliana bila majibu.ingawa si zote za aina hii huwa mbovu. Kikubwa ni kumtanguliza mwanzilishi wa ndoa aikarabati nae ni Muumba.

6⃣ Triangle Marriage.(Ndoa ya Pembetatu)

Hii ni Ndoa yenye Uanzishwaji Na Mungu mwenyewe kuweka Upendo wa kweli Ndani ya wawili. Na wakaamua Kupendana Bila Masharti na Mungu mwenyewe akaandaa Mpango wa Kuwakutanisha na Wakishakutana Huwa kuna Hisia Za Upendo wa Kimungu na siyo Tamaa ndani yao.

Upendo huu sio tamaa kwani utawafanya Kuwa na Nidhamu ya Kumhofu Mungu na Kusubiri wakati wake.

Upendo wenye tamaa nyuma yake huwa una madhara ya Watu Kushirki tendo la ndoa kabla ya Harusi au Siku ha Ndoa.
Ni upendo wa Kiwizi wizi. Na wote ambao Walighafirika kabla ya siki ya Ndoa kuna maombi na Kazi yq Kufanya bila Kupuuzia.
Upendo huu wa Kimungu utawafanya wapendao hao kuruhusu Mungu kuwa Msemaji Mkuu katika Mwanzo wa Uhisiano wao,Mwendelezo wa Uhusiano wao na Mwisho wa Uhisiano wao Hadi Kuingia kwenye Ndoa.

Nidhamu na Hofu mbele za Mungu huwatawala wote wawili kwasababu Yuko dereva Makini aitwaye Jehova anawaongoza. Kundi hili la Wanandoa ni wachache sana Na wengi ndoa zao Zinadumu hata kama kutakuwa na Kolugesheni na Ups and Downs.G.O.D huwa anawasaidia Kuvuka salama.

NI MAOMBI YANGU KUWA SOTE TUINGIE KWENYE KUNDI HILI LILILOJAA BARAKA NA FURAHA TELE

7⃣ Suggestion Marriage( Ndoa za Ushauri)

Hii ni ndoa ambayo Mtu anashauriwa na Mchungaji,anashauriwa na Wazazi au Anashauriwa na Baadhi ya ndugu kwamba fulani atakufaa.


USHAURI WA MCHUNGAJI AU MTU YEYOTE UTAKUBALIKA PALE TU -JEHOVA AKIWEKA APPROVAL YAKE.

Kataa ushauri wa Mchungaji hata wa Askofu kama Jehova Umwabuduye Amelikataa.

Samwel Alimuombea Saul Rehema.
Mungu akasema Nimemkataa.

Samwel aliwaona Kaka zake Daudi wanafaa.

Lakino Mungu alipingana na Ushauri wa Samwel Nabii.

Hivyo Ushauri wa Mchungajo siyo Mwisho wa Maelezo.

Take your step to ask GOD for Approval.

8⃣ MRS HUSBAND AND MR.WIFE marriage. (BI.BWANA na Bw.MKE)

Hiyo ni ndoa ambayo msemaji Mkuu katika Uchumba hadi Ndoa ni Mwanamke.
Kichwa cha Mwanamke kinakuwa juu ya kila mtu ndani ya Nyumba.

Mke huwezi kumkaripia Mumewe na Kumwamulia baadhi ya Matukio Mfano.

1. Wewe chukua nguo hizi ukafue.
2. Wewe kwanini hujatandika kitanda.
3. Wewe nini Wewe na Kwanini ni maneno yanatumika sana kwa upande wa mke kwa mumewe.

Kwa ambao bado hawajaingia Ukipata rafiko ambaye akikwambia kitu usipofanya ananuna ujue ana Roho Ya MRS.HUSBAND.

Atataka akukalie kwenye Mabega.

Si ajabu ukute Baba Anaosha vyombo na Mke kakunja Miguu sebuleni anaangalia Filamu.

Si vibaya ukute Mume anaogesha watoto na Mke Kanyoosha Miguu sebuleni.

Ujue hii Ndoa Inasumbuliwa na Roho ya MRS.HUSBAND.

Tutafakari pamoja.
 
Huu uzi wanajamii hamuuoni au ndio jiwe gizani?
Nimeuweka tujadili ukweli wa Huu uchambuzi wa aina za ndoa. Isije kuwa mwandishi aliandika tu bila kuwa na uhakika.
Tujadiliane wanajamii ikiwa kweli au si kweli.
 
Hongera mtumishi zidi kuiombea ukiziombea na za wengine ambao kwa kujua au kutokujua waliingia kimakosa. Mungu ni mwaminifu atawarehemu na kuwapa amani tele
 
Kuna asilimia kubwa ya ukweli kuhusu huu uchambuzi wa aina za ndoa. Naongezea aina nyigine ya ndoa.

9.Ndoa ya bahati mbaya? Ndoa ambayo watu wanaoana ili tu waonekane mbele ya Jamii kuwa nao ni wanandoa. Hakuna upendo wa dhati. Hii mara nyingi hutokea hasa kwa wanawake pale anapokuwa amekaa muda mrefu bila kupata mtu wa kumwoa. Hukubali kuolewa na mwanaume yeyote anayekuja mbele yake ili aondokane na aibu ya kukaa bila mume.

10. Ndoa ya Ajali. Hii inataka kufanana na. 2. Lakini hii ajali inatokana na kijana kumpa binti mimba na hivyo kulazimishwa kumwoa.

Naishia hapa kwa sasa. Wengine wataendeleza.
 
Back
Top Bottom