AHADI TU-1995,2000,2005,2010 na sasa 2015

AHADI TU-1995,2000,2005,2010 na sasa 2015

specialist88

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2014
Posts
1,140
Reaction score
619
Tz,chini ya CCM haitakaa iendelee kwasababu ahadi za CCM kuanzia 1995,2000,2005 mpaka 2010 zimedhindikana kutekelezeka....

Nina imani kwa miaka yote hiyo ya ahadi juu ya ahadi,ni ahadi nyingi ambazo hazijatekelezwa na kwa uchaguzi huu CCM wanazihaidi tena ahadi hizo kwa wananchi.

Sasa kwa uzi huu,naomba JF member's,popote ulipo ndani ya nchi hii,hebu leta ahadi ambayo unaisikia kwa uchaguzi wa mwaka huu tena ikiahidiwa na CCM japo kuwa walikwisha ihaidi katika chaguzi za mwaka 1995,2000,2005 na 2010 na wakashindwa kuitekeleza.
 
Wingi wa ahadi ni kudhihirisha namna siasa za chama tawala zimekuwa za kitapeli,naona wagombea wanasahau kusimama katika ilani ya chama chao badala yake wanapanda majukwaani na ilani zao binafsi kutapeli wapiga kura! Ngoja tuone mwaka huu!
 
hili swala ndio linalompa umaarufu Lowasa,yeye haongei sana wala nini!!
 
Ahadi za JK kwenye kampeni za kusakaurais 2010
============================

1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora

2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini

3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria- Igunga

4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga

5. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma

6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini

7. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma

8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera

9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi- Kagera

10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba- Bukoba Mjini

11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini

12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera

13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera

14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu- Kagera

15. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya

16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba- Kagera

17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali

18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika- Mwanza

19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza

20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita

21. Kulinda muungano kwa nguvu zote- Pemba

22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro

23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa- Mbeya mjini

24. Kujenga bandari Kasanga ¨CRukwa

25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea

26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya

27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga

28. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa

29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani ¨CKihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro

30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini

31. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora

32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu

33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini

34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)- Hydom Manyara

35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa-Musoma

36. Kulinda haki za walemavu- Makete

37. Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini

38. Kujenga barabara Musoma¨CMto wa Mbu Arusha-Arusha

39. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini

40. Kujenga barabara ya lami Manyoni- Kigoma¨C Kaliua,Tabora

41. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi- Arusha Mjini

42. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma

43. Kuwafidia wanakijiji ng¡¯ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido

44.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga

45. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha ¨C Arusha mjini

46. Kukopesha wavuvi zana za kilimo- Busekera, Wilaya ya Musoma, .

47. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido

48. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti ¨C Ngorongoro

49. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara

50. Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini

51. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa

52. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa

53. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania- Iringa

54. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda

55. kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara

56. kuwapa wanawake nafasi zaidi- Kilolo ,Iringa

57. ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar

58. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa- Kabandamaiti mjini Zanzibar

59. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti

60. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma

61. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma

62. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) ¨CRuvuma

61. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania ¨CRuvuma

62. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam

63. Mtwara kuwa mji wa Viwanda ¨CMtwara

64. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha

65. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa- Kibaha

66. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha
 
Alafu bado wanaendelea kuhaidi tena?!!!kwanza watekeleze hizi
 
Imekula kwenu, shule za kata zimetufumbua macho wasomi ni wengi sasa, hatudanganyiki na ahadi zenu za kofi, tshet, khanga, madera na ahadi zenu za uongo, watoto washule hatudanganyiki tunataka mabadiliko.
 
Back
Top Bottom