Africa Confederation Cup: Sagrada vs Yanga at Nelson Mandela Stadium

Wonderful

JF-Expert Member
Apr 8, 2015
7,348
5,977
13245469_236701226709663_8926825404710683968_n.jpg

FULL TIME: SAGRADA ESPERANCA 1-0 YANGA SC.
YANGA ANASONGA MBELE KWA MATOKEO YA JUMLA YA SAGRADA ESPERANCA 1-2 YANGA SC.

KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA ESPERANCA KATIKA MJI WA DUNDO NCHINI ANGOLA. MECHI ITACHEZWA SAA 9 KWA ANGOLA NA 11, SAA ZA AFRIKA MASHARIKI.

1. Deogratius Munishi
2. Juma Abdul
3. Oscar Joshua
4. Vicente Bossou
5. Nadir Haroub
6. Mbuyu Twite
7. Simon Msuva
8. Thabani Kamusoko
9. Amisi Tambwe
10. Donald Ngoma
11. Haruna Niyonzima

BENCHI:

1. Ally Mustafa
2. Mwinyi Haji
3. Kelvin Yondani
4. Deus Kaseke
5. Geofrey Mwashiuya
6. Mateo Anthony
7. Paul Nonga

==============

2b0c0a38-3686-462f-9803-53b2c36662af.jpg


Mechi imeanza kwa kasi sana, Esperanca wanaonekana wamepania kupata bao la mapema ili kuwachanganya Yanga.

Ngoma anaanguka baada ya kufanyiwa madhambi, lakini inaonekana mwamuzi hajali, mechi inaendelea kwa dakika mbili zaidi.

Dida naye anaanguka hapa baada ya kupangua mpira, inaonekana aligongwa. Kama kuna njama hivi ya kutaka kuwaumiza baadhi ya wachezaji au kuwatafutia kadi

-Kamusoko tayari kalambwa kadi ya njano, Yanga inabidi wawe makini kwa kuwa inaonekana wazi mwamuzi kama anatafuta kadi nyekundu

Dk 24, inaonekana wachezaji wa Esperanca wamepania kuwafanya wa Yanga wapanik

Dk 25, Esperanca wanapata bao kupiria mshambuliaji wao mkongwe Love Kabungula aliyeunganisha krosi baada ya mabeki Yanga kushindwa kuuwahi mpira

BAO

Dida analambwa kadi ya njano, haikuwa sahihi lakini inaonekana baadaye kuna mchezaji wa Yanga atalambwa kadi nyekundu maana mwamuzi anaitengeneza mapema. Dida aliomba kurudishiwa mpira na waokota mpira waliung'ang'ania, mwamuzi kasema alizozana nao.

Dk 41 sasa, mpira unaonekana kubalansi ingawa Yanga wamekuwa wakishambuliwa zaidi

Dk 42 hadi 44 Yanga walionekana kuamka na kupiga pasi nyingi. Hata hivyo hawakufanya mashambulizi makali sana. Inaonekana wanakuwa makini sana ili wasifungwe bao tena

HALF TIME:

Kipindi cha pili kimeanza, Esperanca wanaonekana kuanza kwa kasi wakipania kupata bao la pili. Lakini Yanga nao wanasukuma mashambulizi

Dk 53 sasa, mechi inakwenda kwa kasi sana na Yanga bado wanaonekana kuchangamka

Dk 58, Ngoma yuko chini, anaonekana kuwapa wakati mgumu sana. Wachezaji Yanga na wale Esperanca wanazozana sana hapa

Dk 64 sasa, kidogo Yanga wanaendelea kucheza pasi za haraka, ingawa Sagrada pia wanashambulia mara kwa mara. Dida anaonekana kuwa makini zaidi

Dk 71, Sagrada wanashambulia zaidi. Sasa wanabadilisha kutoka mipira ya krosi na kupiga ile ya chini wakitaka kupenyeza katikati ya uwanja

Dk 73, Ngoma anatolewa tena kwenda kutibiwa nje, hii ni mara ya nne.

Dk 75, Ngoma anageuka na kupiga shuti vizuri lakini linapaa juu kidogo

Sasa ni Dk 78, mpira bado unaonekana ni mashambulizi ya zamu. Yanga wawe makini na washambuliaji wa Sagrada, wanaonekana kulazimisha kutaka kuingia kwenye boksi. Wakifanikiwa ni rahisi kwao kufunga au kujiangusha

Dk 83, Mechi ni ngumu bado, Yanga wanaonekana kuongeza ulinzi zaidi, kingine wanapaswa kujilinda na fauloSasa bado Dk 10 tu, Yanga wanalazimika kuendelea kuweka ulinzi makini zaidi. Kaseke anaonekana kuwa msaada katika ukabaji

Dk 85, Ngoma kaumia, anabebwa na kutolewa nje na machela, lakini wanaonekana kumkimbiza harakaharaka, hali inayosababisha mzozo kidogo

KADI Dk 86 Cannavaro analambwa kadi nyekundu

PENAAAAAAT Dk 87,Wanapata penati baada ya Cannavaro kumwangusha mshambuliaji aliyekuwa anaingia langoni

Fujo zimetawala, vurugu uwanjani hadi polisi wameingia

Wapigapicha kutoka Tanzania wako jukwaani wamefuatwa na kuzuiwa kupiga picha

Penalti inapigwa hapa, Dida anaokoaaaaaaaaaa
Dk 89, Anaingia Yondani, anatoka Tambwe

Sasa ni Dk ya 90

Mwamuzi bado hajaonyesha kibao cha muda wa nyongeza, mzozo unaendelea hapa uwanjani. Haijulikani hata nini kitafuatia, tutaendelea kuwajuza

Dk 90+7 Anaingia Mwashiuya kuchukua nafasi Msuva

Kipa Dida wa Yanga yuko chini anagaagaa baada ya kupigwa jiwe na shabiki aliye nyuma ya lango

90+8

MPIRA UMEKWISHAAAAAAAA

Yanga anasonga mbele kwa matokeo ya jumla ya 2-1.
 
KIKOSI Sagrada esperanca:

Sagrada Esperanca;
Yuri Jose Tavazes,
Roadro Juan da Semero,
Dennis Conha Morais,
Asenio Cabungula,
Antonio da Silva Oliveira,
Ntaku Zabakaka,
Manuel Paulo Joao,
Alentua Tangala Rolli,
Osvaldochitumba Palana,
Manuel Sallo,
Antonio Kasule.
 
Tv ipi itakayorusha live hii mechi wadau?
Sidhani kama kuna TV itakayo rusha, maana Sagrada hawakutaka ata picha mnato zipigwe mpaka viongozi wa Yanga walipoingilia kati kwamba ni mpiga picha wa klabu ya Yanga ingawa yeye alikua mwandishi wa gazeti la champion.
 
KIKOSI Sagrada esperanca:

Sagrada Esperanca;
Yuri Jose Tavazes,
Roadro Juan da Semero,
Dennis Conha Morais,
Asenio Cabungula,
Antonio da Silva Oliveira,
Ntaku Zabakaka,
Manuel Paulo Joao,
Alentua Tangala Rolli,
Osvaldochitumba Palana,
Manuel Sallo,
Antonio Kasule.

Wazambia na Wacongo ndio wamejaa kwenye hiyo timu
 
Sidhani kama kuna TV itakayo rusha, maana Sagrada hawakutaka ata picha mnato zipigwe mpaka viongozi wa Yanga walipoingilia kati kwamba ni mpiga picha wa klabu ya Yanga ingawa yeye alikua mwandishi wa gazeti la champion.
Kwa hiyo hairushwi live?
 
TPA TV ANGOLA wapi live Esperanca vs YANGA
 

Attachments

  • IMG-20160518-WA0032.jpg
    IMG-20160518-WA0032.jpg
    45.2 KB · Views: 102
  • IMG-20160518-WA0031.jpg
    IMG-20160518-WA0031.jpg
    37.2 KB · Views: 112
hao jamaa wana fitina sana sisi tunawachukulia poa wao mpiga picha hawamtaki kuingia uwanjani...
 
Back
Top Bottom