Aden Rage unatuchanganya wana Simba

Aden Rage unatuchanganya wana Simba

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,393
mwenyekiti wa Simba leo akiongea kwenye kipindi cha michezo cha Radio 0ne amesema mchezaji Emmanuel Okwi alishasaini mkataba wa makubaliano na Etoile du sahel mara baada ya kufikisha miezi sita ya mkataba wake, kwaiyo simba ikabidi itumie akili ya kuzaliwa ili kuweza kumuuza na Simba kupata pesa la sivyo Okwi angeondoka bure mwisho wa msimu. Na akili iyo ya ziada bado haijalipa maana bado hawapewa pesa zao na Etoile du sahel aliongeza Rage.
Lakini kwa kumbukumbu zilizopo Okwi alisaini mkataba mpya wa miaka miwili na Simba wakati wa michuano ya CECAFA nchini Uganda. Sasa mheshimiwa Rage ule mkataba ulikuwa na maana gani kwa Simba? ,ilikuwaje mumsahinishe mkataba mpya wakati mnajua alishasaini makubaliano ya awali na Etoile na sheria ilikuwa inamruhusu? Na inaonekana Etoile du sahel hawana wasiwasi na hili swala. Unatuchanganya kwa kweli
 
Huyu jamaaa ujuaji mwiiiingi,mwisho wa siku tunapigwa bao,step down wewe mtu, tumechoka ngonjera zako.
 
Hv Mwana'simba anayemjua Rage vizuri kwl? Cdhani!
 
Huyu jamaaa ujuaji mwiiiingi,mwisho wa siku tunapigwa bao,step down wewe mtu, tumechoka ngonjera zako.

Hapo ndo ninapowapenda washabiki wa timu ya Wananchi, kungekuwa kushanuka zamani sana.
 
Mtu aliyeiba FAT miaka nenda miaka rudi halafu bado Wazee wa Droo mkamkabithi Uenyekiti...

Acha aendelee kutafuna vijisenti kama hivyo kwa kuwa kawapata mazuzu.
 
ukiyashangaa ya Rage utayaona ya kina akilimali..
 
Fedha za Okwi alisha vuta na kununulia malori.
 
ukiyashangaa ya Rage utayaona ya kina akilimali..

Bila kusahau kuyashangaa ya Wateule waongoza team ya Bwana S.S. Bakhresa ambao kila wkt wanamtimua Hall na baadaye kumrudisha
 
Kama unachanganyikiwa Simba,hamia Kandambili. Simba damu wenyewe tunaelewa kila jambo lina muda wake!Ndoo maana muda wa kupata mshiko wa Ngasa ulipofika ilibidi dogo auteme mzigo, Japo aliendelea kulialia oooh wamefoji!! Akaambiwa we tusikusikie unarudia neno hilo! kweli mpaka leo hajarudia tene kusema wamefoji!!! Chezea Simba wewe!!!
 
Kama unachanganyikiwa Simba,hamia Kandambili. Simba damu wenyewe tunaelewa kila jambo lina muda wake!Ndoo maana muda wa kupata mshiko wa Ngasa ulipofika ilibidi dogo auteme mzigo, Japo aliendelea kulialia oooh wamefoji!! Akaambiwa we tusikusikie unarudia neno hilo! kweli mpaka leo hajarudia tene kusema wamefoji!!! Chezea Simba wewe!!!

wewe utakuwa Rage
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom