wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,931
- 4,549
Kampuni ya ACACIA Bulyanhulu kupitia kitengo chake cha Community imeamua kwa ukatili kabisa kuwatoa kwa nguvu wafanyakazi wake kwenye nyumba walizokopeshwa na kampuni hiyo kwa kutumia majembe auction mart ambao kuanzia leo jioni wameanza zoezi hilo lisilo na chembe hata ya ubinadamu,cha kushangaza kampuni kubwa kama ACACIA inashindwa kuwalipa kwanza wafanyakazi walioacha kazi mafao yao ya nyumba ili itaifishe nyumba hizo kwa haki,kampuni hii imekuwa na tabia ya kibabe kwa kiburi cha pesa za dhahabu,inauma sana mtu kumtolea vyombo nje wakati bado anadai pesa nyingi za nyumba,hii ni laana kubwa sana,familia zina watoto wadogo,mvua zinanyesha kwa wingi watu wakaishi wapi? niliyoyaona leo nimesikitika sana kiasi cha kukumbuka maneno ktk kitabu cha mwalimu mkuu wa watu kuwa,ni afadhali ya serikali ya wanyama na ndege kuliko serikali ya binadamu maana hatuna huruma hata baina yetu,ACACIA haina sababu za msingi za kutesa watu hivyo maana hakuna anayehamia ktk nyumba hizo zaidi ya kubaki mahame tu, ni ukatili sana.