Katika kila kijiji, mitaa na miji ya Tanzania, kuna kilio kinachoumiza mioyo ya wengi, lakini hakuna anayekisikia. Ni kilio cha wazazi waliokatishwa tamaa, wakiona vijana wao wakiteketea katika wimbi la pombe kali zinazouzwa kiholela. Vijana waliopaswa kuwa nguvu kazi ya taifa, faraja ya wazazi...