Vilio na simanzi vimetawala kwa wakazi wa Kolandoto mkoani Shinyanga, baada ya watu wawili kuuawa kwa kukatwakatwa na kitu chenye ncha kali na kijana anayesadikiwa kuwa na matatizo ya akili na kujeruhi watu watatu na kisha wananchi wenye hasira kali kumuua muuaji huyo.