Kiukweli kama unahitaji usafiri kwa ajili ya kufika na kurejea mahala aheri ufanye subira aidha kwa kuendelea kudunduliza uweze kujazia hiyo pesa walau ufikishe 5m utafute Passo yako iliyonyooka au Vitz, ama uamue kuchukua bodaboda yako kama TVS, Boxer au nyinginezo uweze kusogeza siku mpaka...
Amejaribu kukuonesha yeye ni mkongwe kiasi gani katika pikipiki. Sio kila anaeendesha pikipiki ana uwezo wa kumudu 1200Cc, ndio maana ametumia hiyo kwa msisitizo. Lugha hizi huwezi elewa kama wewe si muumini wa pikipiki na sio bodaboda.
Wote wanaomiliki pikipiki kubwa hawawazi hivyo vi-baby walker, unakuta wanavyo uwani na hawavipandi wala kuviendesha kwa sbb ya mahaba na pikipiki. Na ukiona mtu anaweka 13m kwenye pikipiki ujue hiyo ni chenji haina matumizi.
Kaka tatizo sisi tunaozipata kwa kuungua jua na kunyeshewa mvua tuna hasira sana, ingekuwa zinakuja kwa ulaini wala isingekuwa tatizo, ingekuwa ni kugawana neema tu, lakini sasa jinsi tuzipatavyo ni mtihani ndio maana tuna hasira sana!
Yaani ndio hivyo hivyo, na sijui ni nani aliebuni mbinu ya kuweka hawa wahudumu wa jinsi ya kike, maana akijichekesha tu unamsamehe, mimi nimeshikwa sana na hasira asubuhi, nikatamani kumpa walau kelbu mbili aamke, nikawaza jela, nikakumbuka familia yangu nikajikuta narudisha moyo nyuma!
Mimi huwa naumia sana roho nikigundua haya ya uharibifu.
Najiuliza sana maswali yasiyo na majibu: Hivi akili hizo wanazotumia hawa vibaka kuturudisha nyuma kwanini wasizitumie katika ubunifu wa mambo yenye kunufaisha jamii?!
Tatizo ni kucheza na budget, mimi TVS yangu huwa najua nikiweka mafuta ya elfu 30 natumia wiki 2, sasa nikisema niweke nusu nusu nakuwa najitega mwenyewe, halafu nina imani kuwa tank ukilijaza mafuta ya kutosha unatunza pump, unalitunza tank lenyewe, unaboresha matumizi ya mafuta na performance...
Kwa hesabu za haraka haraka ni kwamba: anaibiwa mwenye kituo cha mafuta kwa sbb yale mafuta yameuzwa bila mashine ya risiti kurekodi, pia anaibiwa mwenye chombo anaewekewa mafuta maana analipia mafuta ambayo hakuwekewa! Hii kwa kifupi inaitwa DOUBLE IMPACT!
Tatizo la kidumu kaka unakuwa unarisk maisha yako lakini pia huwezi kuwa na chombo cha moto halafu ukafika kituo cha mafuta ukashuka na kidumu wakati tank lipo na linafunguka! Hii mbinu ni nzuri sana kama upo kwenye dharula.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.