Jamii forum kuruhusu mijadala kama hii ni hatari. Jamii zetu zimechangamana sana. Unakuta baba muislam mama mkiristu. Na hatujaeahi kuona shida.
Sasa kama mijadala ya msingi imetushinda bora tukae kimya. Hizi dini tumeketewa tusisahau historia. Na bado kuna mataifa makubwa na yameendelea...
Mbona watu mna wivu usio na ticha? Kabla yake ni nani alikuepo na akafanya nini? Haya kashatolewa nishati, je mmepata umeme? Tuepuke personality unapokua na matatizo yako usihamishie chuki zako kwa mtu. Serikali ni mifumo na si mtu mmoja. Sina interest na huyu mtu ila nimekua nikiona mara nyingi...
We ni mpumbavu sana. Kwanini unakashfu dini za wenzako kwa hoja dhaifu. Hivi kwenu dunia au tanzania tunayoishi ni yakubaguana na kukashfiana kiasi hiki? Unadhani waislam wanajisikiaje wakisoma utumbo kama huu? Kwanini JF mtu kama huyu asidhibitiwe? Yawezekana we mwenyewe ni zao muislam siri...
Kuwa muelewa digrii ya heshima haisomewi wala haina mahusiano na ya kusomea, hata angekua madarakani huyo slaa. Ni standard za kimataifa hata msanii anaweza kupewa msipotoshe watu jamani
kumbe unasikia. Si vyema kuongea jambo ambalo hujalifanyoa utafiti. Bublication sio siri mtu yeyote anaweza kusrarch ili kukuprove wrong. Siamini kama kweli we ni msosi unatoa povu tu
kinachoangaliwa ni sifa. Kama ana sifa kuwa na ndugu serikalini si kosa kwani wote waliopata ndugu zao ni maafisa serikalini. Tusiwanyime watu haki zao jamani
Ukiangalia udini kwa mtindo huo utakua umepotoka. Hatuitaji kujua fulani anaeongoza taasisi fulani ni dini gani. Pia wewe utakua unatumia kigezo cha majina ukifikiri huo ndio udini.
Mtu anayejikita sana kwenye udini namchukia sana. Watu wanalalamikia udini ukiangalia mijadala hata ya jf baadhi wanajikita kwenye kuukuza. Tena kwa kutojua wajatafsiri udini kwa kuangalia jina la mtu. Akiona halitumiki kwenye dini yake anamvamia mtu. Udini si majina pevukeni jamani. Eleza mtu...
Vipi kuhusu familia za waliouwawa hazitajumuishwa kwa namna yoyote ile kwenye maazimisho hayo? Nafikiri ingekua ni vyema kama nao wangekumbukwa kwani walipoteza watu muhimu
Hiyo lugha unayotumia inakutambulisha we ni nani. Badala yakupandisha chati chama inaweza kutia doa kwa wanachama na mashabiki. Jifunze kutumia mitandao ya kijamii kiungwana. Ulishaanza kumshambulia mtu ukiambiwa bahati mbaya kalazwa au hayuko nchi. We unafikiri watu wanaishi kwa midahalo tu?
kwa kauli unazotumia sidhani kama ni za kujenga. Huwezi kutumia lugha kama hii ukajiita mkombozi au shabiki wa chama zaidi ya kufanya watu waone chama kimejaa wahuni kama wewe! Kulikua na ulazima gan wakutumia lugha kama hii. Jifunze kuongea hiyo sio siasa unayofanya.
Nasikitika hata wale mnaojiona mnafaa mnachokijadiri humu ni kinyaa. Mnajadili watu kwa maeneo wanakotoka, mama zao, baba zao na makabila yao. Sasa sijui vitu hivi vimekua kigezo cha kumpata kiongozi bora tangu lini?
Acha ushabiki wa kijinga, mhusika anakwambia hakua na taarifa we unabisha. Kumbuka siku ile ya mjadala Zitto alitoka kabla mjadala haujaisha akawambia ana safari. Pia nae ni binadam kwani unajua kupatwa nini asubuhi? Ndo tatizo la kushabikia siasa ukubwani. Achana na mawazo finyo kwani huyo zito...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.