Hakushikwa Kenyata, japo alikwenda huko walikomuita ICC, Eti aje akamatwe Samia.
Acheni ndoto za mchana.
Mtaoumia ni nyie wananchi, kwa maana akisaini mkataba mmoja tu wa Gesi ya Mtwara, hapo hakuna cha ICC wala uchafu mwingine.
ICC ipo pale kwa ajili ya kuwashibisha/maslahi ya wazungu, sio...
Uchaguzi na utekaji umezaliwa mwaka huu tu, du hatari. Katiba ile ile iliyotumika mwa 2020 sijui ndio inatumika leo au ni nyingine. Mwaka 2020 hawa walikaa kimya.
Tatizo sio Samia bali ni mfumo.
Yalikuwepo hayo wakati wa Mkapa, Kikwete na hata Magufuli.
Sijui kwa nini vijana mnataka kuzima data zetu utafikiri mnayemlaumu ni Rais toka chama tofauti na watangulizi wake.
Kuna watu wanazima data zao na kukomalia kuwa tatizo ni Rais Samia Suluhu Hassan. Na kukazia zaidi kuwa "Hatumtaki Samia" Mimi najiuliza Hivi uchaguzi ulikuwa wa haki wakati wa Mkapa, Kikwete, Magufuli....... Je Samia ndio alikuwa anafix nyakati hizo zote. Amkeni na muelewe tatizo lilipo.
Wewe ndio ulizungumzia kushinda vita, rejea hoja yako namba #18. Kifupi umenielewa, na nakushukuru kwa hilo.
Kwa bahati nzuri umenisaidia hapa, sina nyongeza.
Naelewa kuwa kumgusa T. Lissu, utatupiwa mawe sana. Lakini kwa sababu suala lenyewe linahusu Taifa kwanza, nipo tayari kujibu mapigo. Ukweli ni kwamba kuandamana kwa ajili ya TL sipo tayari, na wala si taki mtu ashawishike kufanya hivyo kama walivyofanya 2020 alipowamba wananchi waandamane.
Mmmmm! Nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa Lissu ni next level. Kwangu ni hao hao tu kama akina M7. Kabla ya kuingia madarakani alinena kuwa tatizo la viongozi/marais wa Afrika ni kukaa sana madarakani. Ulipofika wakati wake akawa anabadili maneno tu, na sasa ni moja kati ya viongozi waliokaa sana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.