Katibu mkuu wa Baraza la Mawazi Zambia Bw. Patrick Kangwa ametembelea banda la Tanzania katika Maonesho ya 98 ya Kilimo na Biashara Zambia na kupongeza uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya Afya Tanzania na kuahidi ushirikiano zaidi katika ueekezaji na biashara katika sekta ya Afya
Washiriki wa Maonesho ya 98 ya kilimo na Biashara Zambia wameendelea kutembelea banda la Tanzania na kujifunza kuhusu huduma za kibingwa na kibobezi zinazotolewa na Taasisi ya MOI, MZRH pamoja na huduma za Uchukuzi na Usafiri za Mamlaka ya Bandari Tanzania na Shirika la ndege la Tanzania.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais (Baraza la Mawaziri Zambia) Prof. Lackson Kasonka atembelea banda la Tanzania katika Maonesho ya 98 ya kilimo na biashara Zambia, apongeza huduma za kibingwa na kibobezi zinazotolewa na Taasisi ya MOI na MZRH
Prof. Lackson Kasonka, Katibu Mkuu (SD) kutoka Ofisi ya Rais (Baraza la Mawaziri) Zambia, akipokea zawadi kutoka kwa Prof. Reuben Mutaganywa (Daktari Bingwa Mbobezi MOI) baada ya kutembelea banda la Tanzania katika Maonesho ya 98 ya kilimo na biashara nchini Zambia
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga hatua nyingine kubwa katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi na Tiba Utalii (Medical Tourism), kufuatia kuwasili kwa jopo la madaktari bingwa na mabingwa bobezi nchini Zambia kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (MZRH)...
Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili MOI inashiriki kwa mara ya pili katika Maonesho ya Elimu ya Juu yanayofanyika viwanja vya Gombani, Pemba kwa lengo la kuwafahamisha wananchi juu ya huduma za kibingwa na kibobezi zinazopatikana nchini.
Ushiriki huo unalenga kupunguza idadi ya...
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Paul Makonda, ameipongeza Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili - MOI kwa kuanzisha kambi maalum ya matibabu ya kuwahudumia wananchi wa Arusha na mikoa jirani.
Mhe. Makonda ametoa pongezi hizo leo...
Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeendelea kutoa huduma za kibingwa na kibobezi kupitia madaktari wake bingwa na bobezi wa mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu katika kambi maalum ya matibabu inayoendelea mkoani Arusha.
Wananchi wa Mkoa wa Arusha na mikoa jirani...
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, amepongeza huduma za kibingwa na kibobezi zinazotolewa na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba, huku akihimiza kuendelea kuimarishwa kwa kampeni ya "Vaa Helmeti, Ubongo...
Huduma za kibingwa na kibobezi za Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) zimeendelea kuvutia wananchi katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Kupitia maonesho hayo, MOI imesogeza huduma karibu zaidi na wananchi kwa kuendesha kliniki maalum ya...
Wauguzi wa Chumba cha Upasuaji kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) wameendelea kupatiwa mafunzo ya kuwakumbusha misingi na kanuni za matumizi sahihi ya vipandikizi vinavyotumika katika matibabu ya mivunjiko ya mifupa, ikiwa ni sehemu ya programu endelevu inayodhaminiwa na...
Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeshiriki katika Mkutano wa 3 wa Kimataifa wa Kimkakati wa Kikanda wa PEN-PLUS unaolenga kujadili na kuimarisha mikakati ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza, unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC)...
Jumla ya wananchi 537 wamepatiwa huduma za kibingwa na kibobezi katika banda la Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Maadhimisho hayo yamehitimishwa leo, Juni 23, 2026 na...
Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeeleza mpango wake wa kuanzisha huduma mpya mbalimbali za kibobezi zitakazoifanya kuendelea kuwa kitovu cha weledi cha matibabu ya mifupa na mfumo wa fahamu katika ukanda wa Afrika.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 30...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.