Na kwa nini yote hayo yatokee kama mhusika ana haki ya ushindi 😂?
Kwamba TGB na Pigabet wajinga sana mpaka wapoteze muda wao kukaa na mtu asiyestahili kulipwa?
Eti hana ushahidi kwa hiyo hizo screenshot amezitolea wapi?
Unadhani hao bodi wangethubutu hata kumsikiliza kama hana ushahidi?😂🙌
Utetezi wako dhaifu sana bro acha kutetea dhurma
Una uhakika gani? Je kama aliscreenhot mapema kama ushahidi wa lolote linaloweza kutokea? Halafu kumbe hujaelewa mtoa mada anazungumzia kufutwa kwa mkeka baada ya kushinda na sio wakati game zikiendelea
Msingi wa hoja yako sio sahihi kwa mtoa mada kwa sababu wewe ulikimbilia kumuattack badala ya kuangalia muktadha upande wake upoje
Muktadha kwake ashasema walikubali kumlipa lakini kwa kiwango pungufu bila sababu za msingi ambacho kwake bado anaona sio sahihi, huoni kama mpaka tayari hoja zako...
Halafu mbona iko wazi kampuni uchwara zinajulikana
Ndiyo maana ukiuliza watu wanaobeti kuhusu kampuni zinazoaminika huwezi kukuta kuna mtu hata mmoja kataja hiyo kampuni yako uchwara .
Watakutajia
1. BetPawa
2. Betway
3. Sportybet
4. Sportpesa
5. Premierbet
Ni vile sio mwanasheria ,but naamini wadau wengi tumeshauri atafute jopo la wanasheria na mawakili akifata ushauri atapata stahiki yake
Na wewe mbona umetoa jibu la swali moja wakati nimeuliza matatu hayo mbona hujayajibu 😂
Ngoja nirudie labda hukuyaona
Anyway sasa jamaa wanataka wamlipe...
Ndo maana nikatetea utetezi wangu kuonesha kuwa kampuni ina janja janja nyingi na ukurupukaji .
Hiyo kampuni yako ilikuwa inafikia kipindi mtu unadeposit hela leo ila inaingia keshokutwa tena baada ya kupiga sana simu customer service
Inshort Bongo kampuni uchwara kama hizi zinajulikana
Anyway sasa jamaa wanataka wamlipe mililion 3 ili iweje?
Na kama kuna hivyo visababishi kwa nini bet ilikuwa won na hakuna pingamizi lolote walioliweka?
Kama kakosea kwa nini wanambembeleza ?
Inshort jamaa akitumia wanasheria nguli hiyo kampuni yako ya janja janja mtamlipa fidia kubwa mpaka...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.